< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La sabiduría ha construido su casa, ha preparado sus siete pilares.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Ella ha sacrificado a sus animales para obtener su carne; ha mezclado su vino y ha alistado la mesa.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Ha enviado a sus siervas con invitaciones. Llama desde los lugares altos de la ciudad, diciendo:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
“¡Todos los que necesiten aprender, vengan a mi!” A los insensatos les dice:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
“Vengan, coman mi carne y beban del vino que he mezclado.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Dejen de vivir con necedad, y sigan el camino de la sensatez”.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Si corriges al burlador, recibirás insultos; si corriges al malvado por lo que hace, recibirás abuso.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Por lo tanto, no discutas con los burladores, pues solo te odiarán; discute con el sabio y te amará.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Educa al sabio y se volverá más sabio. Enseña a los que viven en rectitud y aumentarán su conocimiento.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
El principio de la sabiduría es honrar a Dios. Y el conocimiento del Santo trae inteligencia.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Mediante la sabiduría vivirás muchos años más. Añadirás años a tu vida.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si eres sabio, tú obtendrás los beneficios de la sabiduría, pero si eres un burlador, solo tú sufrirás las consecuencias.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
La estupidez es como una mujer escandalosa e ignorante.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
Esa que se sienta en la puerta de su casa, se sienta en los lugares altos de la ciudad,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
llamando a los que pasan, involucrándose en asuntos ajenos, y diciendo:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
“¡Los que necesiten aprender, vengan a mi!” A los necios les dice:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
“El agua robada es dulce, y la comida que se come en secreto sabe mejor!”
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
Pero ellos no saben que los Muertos están con ella, que aquellos a quienes ella ha invitado antes están en lo profundo de una tumba. (Sheol )