< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
A verdadeira sabedoria edificou sua casa; ela lavrou suas sete colunas.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Ela sacrificou seu sacrifício, misturou seu vinho, e preparou sua mesa.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Mandou suas servas, [e] está convidando desde os pontos mais altos da cidade, dizendo:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Qualquer um que for ingênuo, venha aqui. Aos que têm falta de entendimento, ela diz:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Vinde, comei do meu pão; e bebei do vinho que misturei.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Abandonai a tolice; e vivei; e andai pelo caminho da prudência.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Aquele que repreende ao zombador, toma desonra para si mesmo; e o que tenta corrigir ao perverso acaba sendo manchado.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Não repreendas ao zombador, para que ele não te odeie; repreende ao sábio, e ele te amará.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Ensina ao sábio, e ele será mais sábio ainda; instrui ao justo, e ele aumentará seu conhecimento.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
O temor ao SENHOR é o princípio da sabedoria; e o conhecimento dos santos [é] a prudência.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Porque por mim teus dias serão multiplicados; e anos de vida a ti serão aumentados.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Se fores sábio, serás sábio para ti; e se fores zombador, somente tu aguentarás.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
A mulher louca é causadora de tumultos; [ela é] tola, e não sabe coisa alguma.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
E se senta à porta de sua casa, sobre uma cadeira, nos lugares altos da cidade;
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
Para chamar aos que passam pelo caminho, e passam por suas veredas, [dizendo]:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Qualquer um que for ingênuo, venha aqui! E aos que tem falta de entendimento, ela diz:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
As águas roubadas são doces; e o pão escondido é agradável.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Porém não sabem que ali estão os mortos; seus convidados estão nas profundezas do Xeol. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >