< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
Mądrość zbudowała dom swój, i wyciosała siedm słupów swoich;
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Pobiła bydło swoje, roztworzyła wino swoje, i stół swój przygotowała;
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
A rozesłała dzieweczki swoje, woła na wierzchach najwyższych miejsc w mieście, mówiąc:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Ktokolwiek jest prostakiem, wstąp sam; a do głupich mówi:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Pójdźcie, jedzcie chleb mój, i pijcie wino, którem roztworzyła.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Opuśćcie prostotę, a będziecie żyli, a chodźcie drogą roztropności.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Kto strofuje naśmiewcę, odnosi hańbę; a kto strofuje niezbożnika, odnosi zelżywość.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Nie strofuj naśmiewcy, aby cię nie miał w nienawiści; strofuj mądrego, a będzie cię miłował.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Uczyń to mądremu, a mędrszym będzie; naucz sprawiedliwego, a będzie umiejętniejszym.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Początek mądrości jest bojaźń Pańska, a umiejętność świętych jest rozum.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Bo przez mię rozmnożą się dni twoje, i przedłużą się lata żywota.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Będzieszli mądrym, sobie będziesz mądrym; a jeźli naśmiewcą, ty sam szkodę odniesiesz.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Niewiasta głupia świegotliwa jest, prostaczka, i nic nieumiejąca;
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
A siedzi u drzwi domu swego na stołku, na miejscach wysokich w mieście,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
Aby wołała na idących drogą, którzy prosto idą ścieszkami swemi, mówiąc:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Ktokolwiek jest prostakiem, wstąp sam; a do głupiego mówi:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
Wody kradzione słodsze są, a chleb pokątny smaczniejszy.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
Ale prostak nie wie, że tam są umarli, a ci, których wezwała, są w głębokościach grobu. (Sheol )