< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
Mądrość zbudowała dom swój, i wyciosała siedm słupów swoich;
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Pobiła bydło swoje, roztworzyła wino swoje, i stół swój przygotowała;
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
A rozesłała dzieweczki swoje, woła na wierzchach najwyższych miejsc w mieście, mówiąc:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Ktokolwiek jest prostakiem, wstąp sam; a do głupich mówi:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Pójdźcie, jedzcie chleb mój, i pijcie wino, którem roztworzyła.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Opuśćcie prostotę, a będziecie żyli, a chodźcie drogą roztropności.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Kto strofuje naśmiewcę, odnosi hańbę; a kto strofuje niezbożnika, odnosi zelżywość.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Nie strofuj naśmiewcy, aby cię nie miał w nienawiści; strofuj mądrego, a będzie cię miłował.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Uczyń to mądremu, a mędrszym będzie; naucz sprawiedliwego, a będzie umiejętniejszym.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Początek mądrości jest bojaźń Pańska, a umiejętność świętych jest rozum.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Bo przez mię rozmnożą się dni twoje, i przedłużą się lata żywota.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Będzieszli mądrym, sobie będziesz mądrym; a jeźli naśmiewcą, ty sam szkodę odniesiesz.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Niewiasta głupia świegotliwa jest, prostaczka, i nic nieumiejąca;
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
A siedzi u drzwi domu swego na stołku, na miejscach wysokich w mieście,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
Aby wołała na idących drogą, którzy prosto idą ścieszkami swemi, mówiąc:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Ktokolwiek jest prostakiem, wstąp sam; a do głupiego mówi:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
Wody kradzione słodsze są, a chleb pokątny smaczniejszy.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Ale prostak nie wie, że tam są umarli, a ci, których wezwała, są w głębokościach grobu. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >