< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
Sapientia ædificavit sibi domum, excidit columnas septem.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Immolavit victimas suas, miscuit vinum, et proposuit mensam suam.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Misit ancillas suas ut vocarent ad arcem, et ad mœnia civitatis:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Si quis est parvulus, veniat ad me. Et insipientibus locuta est:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Venite, comedite panem meum, et bibite vinum quod miscui vobis.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Relinquite infantiam, et vivite, et ambulate per vias prudentiæ.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Qui erudit derisorem, ipse iniuriam sibi facit: et qui arguit impium, sibi maculam generat.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Noli arguere derisorem, ne oderit te. Argue sapientem, et diliget te.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Da sapienti occasionem, et addetur ei sapientia. Doce iustum, et festinabit accipere.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Principium sapientiæ timor Domini: et scientia sanctorum, prudentia.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Per me enim multiplicabuntur dies tui, et addentur tibi anni vitæ.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si sapiens fueris, tibimetipsi eris: si autem illusor, solus portabis malum.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Mulier stulta et clamosa, plenaque illecebris, et nihil omnino sciens,
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
sedit in foribus domus suæ super sellam in excelso urbis loco,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
ut vocaret transeuntes per viam, et pergentes itinere suo:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Qui est parvulus, declinet ad me. Et vecordi locuta est:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
Aquæ furtivæ dulciores sunt, et panis absconditus suavior.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Et ignoravit quod ibi sint gigantes, et in profundis inferni convivæ eius. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >