< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
智慧はその家を建て その七の柱を砍成し
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
その畜を宰り その酒を混和せ その筵をそなへ
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
その婢女をつかはして邑の高處に呼はりいはしむ
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
拙者よここに來れと また智慧なき者にいふ
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
汝等きたりて我が糧を食ひ わがまぜあはせたる洒をのみ
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
拙劣をすてて生命をえ 聡明のみちを行め
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
嘲笑者をいましむる者は恥を己にえ 惡人を責むる者は疵を己にえん
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
嘲笑者を責むることなかれ 恐くは彼なんぢを惡まん 智慧ある者をせめよ 彼なんぢを愛せん
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
智慧ある者に授けよ 彼はますます智慧をえん 義者を教へよ 彼は知識に監まん
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
ヱホバを畏るることは智慧の根本なり 聖者を知るは聡明なり
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
我により汝の日は多くせられ 汝のいのちの年は増べし
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
汝もし智慧あらば自己のために智慧あるなり 汝もし嘲らば汝ひとり之を負ん
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
愚なる婦は嘩しく且つたなくして何事をも知らず
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
その家の門に坐し邑のたかき處にある座にすわり
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
道をますぐに過る往來の人を招きていふ
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
拙者よここに來れと また智慧な在りき人にむかひては之にいふ
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
竊みたる水は甘く密かに食ふ糧は美味ありと
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
彼處にある者は死し者その客は陰府のふかき處にあることを是等の人は知らざるなり (Sheol h7585)

< Mithali 9 >