< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La Sapienza si è costruita la casa, ha intagliato le sue sette colonne.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Ha ucciso gli animali, ha preparato il vino e ha imbandito la tavola.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Ha mandato le sue ancelle a proclamare sui punti più alti della città:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
«Chi è inesperto accorra qui!». A chi è privo di senno essa dice:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
«Venite, mangiate il mio pane, bevete il vino che io ho preparato.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Abbandonate la stoltezza e vivrete, andate diritti per la via dell'intelligenza».
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Chi corregge il beffardo se ne attira il disprezzo, chi rimprovera l'empio se ne attira l'insulto.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Non rimproverare il beffardo per non farti odiare; rimprovera il saggio ed egli ti amerà.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Dà consigli al saggio e diventerà ancora più saggio; istruisci il giusto ed egli aumenterà la dottrina.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Fondamento della sapienza è il timore di Dio, la scienza del Santo è intelligenza.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Per mezzo mio si moltiplicano i tuoi giorni, ti saranno aggiunti anni di vita.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Se sei sapiente, lo sei a tuo vantaggio, se sei beffardo, tu solo ne porterai la pena.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Donna irrequieta è follia, una sciocca che non sa nulla.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
Sta seduta alla porta di casa, su un trono, in un luogo alto della città,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
per invitare i passanti che vanno diritti per la loro strada:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
«Chi è inesperto venga qua!». E a chi è privo di senno essa dice:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
«Le acque furtive sono dolci, il pane preso di nascosto è gustoso».
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Egli non si accorge che là ci sono le ombre e che i suoi invitati se ne vanno nel profondo degli inferi. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >