< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
חכמות בנתה ביתה חצבה עמודיה שבעה
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
טבחה טבחה מסכה יינה אף ערכה שלחנה
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
שלחה נערתיה תקרא-- על-גפי מרמי קרת
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
מי-פתי יסר הנה חסר-לב אמרה לו
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
לכו לחמו בלחמי ושתו ביין מסכתי
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
עזבו פתאים וחיו ואשרו בדרך בינה
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
יסר לץ--לקח לו קלון ומוכיח לרשע מומו
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
אל-תוכח לץ פן-ישנאך הוכח לחכם ויאהבך
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
תן לחכם ויחכם-עוד הודע לצדיק ויוסף לקח
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
תחלת חכמה יראת יהוה ודעת קדשים בינה
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
כי-בי ירבו ימיך ויוסיפו לך שנות חיים
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
אם-חכמת חכמת לך ולצת לבדך תשא
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
אשת כסילות המיה פתיות ובל-ידעה מה
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
וישבה לפתח ביתה-- על-כסא מרמי קרת
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
לקרא לעברי-דרך המישרים ארחותם
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
מי-פתי יסר הנה וחסר-לב ואמרה לו
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
מים-גנובים ימתקו ולחם סתרים ינעם
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
ולא-ידע כי-רפאים שם בעמקי שאול קראיה (Sheol h7585)

< Mithali 9 >