< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
La sagesse s’est bâtie une maison, elle a taillé sept colonnes.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Elle a immolé ses victimes, mêlé le vin et dressé sa table.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Elle a envoyé ses servantes pour appeler ses conviés, à la forteresse et aux murs de la cité:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
Si quelqu’un est tout petit, qu’il vienne à moi. Et à des insensés elle a dit:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
Venez, mangez mon pain, et buvez le vin que je vous ai mêlé.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Quittez l’enfance, et vivez, et marchez par les voies de la prudence.
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Celui qui instruit un railleur se fait injure à lui-même; et celui qui reprend un impie se crée une tache.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Ne reprends pas un railleur, de peur qu’il ne te haïsse. Reprends un sage, et il t’aimera.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Donne à un sage une occasion, et il recevra un surcroît de sagesse. Enseigne un juste, et il se hâtera de recevoir l’instruction.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Le principe de la sagesse est la crainte du Seigneur; et la science des saints est la prudence.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
Car par moi seront multipliés tes jours, et te seront données des années de vie.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Si tu es sage, c’est pour toi-même que tu le seras; mais si tu es moqueur, seul, tu en porteras le mal.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Une femme insensée, criarde, pleine d’attraits et ne sachant absolument rien,
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
S’est assise à la porte de sa maison, sur un siège, en un lieu élevé de la ville,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
Afin d’appeler ceux qui passent par la voie, et qui poursuivent leur chemin:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
Que celui qui est tout petit se détourne et vienne vers moi. Et elle a dit à un jeune homme sans cœur:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
Des eaux dérobées sont plus douces, et un pain caché est plus suave.
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
Et il ignore que là sont des géants, et que dans les profondeurs de l’enfer sont ses convives. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >