< Mithali 9 >

1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
Wisdom has built her house. She has set up her seven pillars.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
She has prepared her meat. She has mixed her wine. She has also set her table.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
She has sent out her maidens. She cries from the highest places of the city:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
"Whoever is simple, let him turn in here." As for him who is void of understanding, she says to him,
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
"Come, eat some of my bread, Drink some of the wine which I have mixed.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Leave your simple ways, and live. Walk in the way of understanding."
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
He who corrects a mocker invites insult. He who reproves a wicked man invites abuse.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Do not reprove a scoffer, lest he hate you. Reprove a wise man, and he will love you.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Instruct a wise man, and he will be still wiser. Teach a righteous man, and he will increase in learning.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
The fear of the LORD is the beginning of wisdom. The knowledge of the Holy One is understanding.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
For by me your days will be multiplied. The years of your life will be increased.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
If you are wise, you are wise for yourself. If you mock, you alone will bear it.
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
The foolish woman is loud, Undisciplined, and knows nothing.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
She sits at the door of her house, on a seat in the high places of the city,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
To call to those who pass by, who go straight on their ways,
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
"Whoever is simple, let him turn in here." as for him who is void of understanding, she says to him,
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
"Stolen water is sweet. Food eaten in secret is pleasant."
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol h7585)
But he doesn't know that the dead are there, that her guests are in the depths of Sheol. (Sheol h7585)

< Mithali 9 >