< Mithali 9 >
1 Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
Mudrost je sazidala sebi kuću, i otesala sedam stupova.
2 Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
Poklala je svoje klanice, pomiješala svoje vino i postavila svoj stol.
3 Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
Poslala je svoje djevojke da objave svrh gradskih visina:
4 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
“Tko je neiskusan, neka se svrati ovamo!” A nerazumnima govori:
5 Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
“Hodite, jedite od mojega kruha i pijte vina koje sam pomiješala.
6 Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
Ostavite ludost, da biste živjeli, i hodite putem razboritosti.”
7 “Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
Tko poučava podrugljivca, prima pogrdu, i tko prekorava opakoga, prima ljagu.
8 Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
Ne kori podsmjevača, da te ne zamrzi; kori mudra, da te zavoli.
9 Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
Pouči mudroga, i bit će još mudriji; uputi pravednoga, i uvećat će se njegovo znanje.
10 “Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
Gospodnji strah početak je mudrosti, a razboritost je spoznaja Presvetog.
11 Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
“Po meni ti se umnožavaju dani i množe ti se godine života.
12 Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
Ako si mudar, sebi si mudar; budeš li podsmjevač, sam ćeš snositi.”
13 Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
Gospođa ludost puna je strasti, prosta je i ne zna ništa.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
I sjedi na vratima svoje kuće na stolici, u gradskim visinama,
15 akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
te poziva one koji prolaze putem, koji ravno idu svojim stazama:
16 Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
“Tko je neiskusan, neka se svrati ovamo!” I nerazumnomu govori:
17 “Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
“Kradena je voda slatka i ugodno je potajno jesti kruh.”
18 Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )
A on ne zna da su Sjene ondje, da uzvanici njezini počivaju u Podzemlju. (Sheol )