< Mithali 8 >

1 Je, hekima haitani? Je, ufahamu hapazi sauti?
知恵は呼ばわらないのか、悟りは声をあげないのか。
2 Juu ya miinuko karibu na njia, penye njia panda, ndipo asimamapo;
これは道のほとりの高い所の頂、また、ちまたの中に立ち、
3 kando ya malango yaelekeayo mjini, kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:
町の入口にあるもろもろの門のかたわら、正門の入口で呼ばわって言う、
4 “Ni ninyi wanaume, ninaowaita; ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.
「人々よ、わたしはあなたがたに呼ばわり、声をあげて人の子らを呼ぶ。
5 Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
思慮のない者よ、悟りを得よ、愚かな者よ、知恵を得よ。
6 Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
聞け、わたしは高貴な事を語り、わがくちびるは正しい事を語り出す。
7 Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.
わが口は真実を述べ、わがくちびるは悪しき事を憎む。
8 Maneno yote ya kinywa changu ni haki; hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.
わが口の言葉はみな正しい、そのうちに偽りと、よこしまはない。
9 Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.
これはみな、さとき者の明らかにするところ、知識を得る者の正しとするところである。
10 Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, maarifa badala ya dhahabu safi,
あなたがたは銀を受けるよりも、わたしの教を受けよ、精金よりも、むしろ知識を得よ。
11 kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.
知恵は宝石にまさり、あなたがたの望むすべての物は、これと比べるにたりない。
12 “Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; ninamiliki maarifa na busara.
知恵であるわたしは悟りをすみかとし、知識と慎みとをもつ。
13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
主を恐れるとは悪を憎むことである。わたしは高ぶりと、おごりと、悪しき道と、偽りの言葉とを憎む。
14 Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu; nina ufahamu na nina nguvu.
計りごとと、確かな知恵とは、わたしにある、わたしには悟りがあり、わたしには力がある。
15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,
わたしによって、王たる者は世を治め、君たる者は正しい定めを立てる。
16 kwa msaada wangu wakuu hutawala, na wenye vyeo wote watawalao dunia.
わたしによって、主たる者は支配し、つかさたる者は地を治める。
17 Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
わたしは、わたしを愛する者を愛する、わたしをせつに求める者は、わたしに出会う。
18 Utajiri na heshima viko kwangu, utajiri udumuo na mafanikio.
富と誉とはわたしにあり、すぐれた宝と繁栄もまたそうである。
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
わたしの実は金よりも精金よりも良く、わたしの産物は精銀にまさる。
20 Natembea katika njia ya unyofu katika mapito ya haki,
わたしは正義の道、公正な道筋の中を歩み、
21 nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.
わたしを愛する者に宝を得させ、またその倉を満ちさせる。
22 “Bwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake, kabla ya matendo yake ya zamani;
主が昔そのわざをなし始められるとき、そのわざの初めとして、わたしを造られた。
23 niliteuliwa tangu milele, tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa.
いにしえ、地のなかった時、初めに、わたしは立てられた。
24 Wakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa, wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji;
まだ海もなく、また大いなる水の泉もなかった時、わたしはすでに生れ、
25 kabla milima haijawekwa mahali pake, kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa,
山もまだ定められず、丘もまだなかった時、わたしはすでに生れた。
26 kabla hajaumba dunia wala mashamba yake au vumbi lolote la dunia.
すなわち神がまだ地をも野をも、地のちりのもとをも造られなかった時である。
27 Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, wakati alichora mstari wa upeo wa macho juu ya uso wa kilindi,
彼が天を造り、海のおもてに、大空を張られたとき、わたしはそこにあった。
28 wakati aliweka mawingu juu na kuziweka imara chemchemi za bahari,
彼が上に空を堅く立たせ、淵の泉をつよく定め、
29 wakati aliiwekea bahari mpaka wake ili maji yasivunje agizo lake, na wakati aliweka misingi ya dunia.
海にその限界をたて、水にその岸を越えないようにし、また地の基を定められたとき、
30 Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake. Nilijazwa na furaha siku baada ya siku, nikifurahi daima mbele zake,
わたしは、そのかたわらにあって、名匠となり、日々に喜び、常にその前に楽しみ、
31 nikifurahi katika dunia yake yote nami nikiwafurahia wanadamu.
その地で楽しみ、また世の人を喜んだ。
32 “Basi sasa wanangu, nisikilizeni; heri wale wanaozishika njia zangu.
それゆえ、子供らよ、今わたしの言うことを聞け、わたしの道を守る者はさいわいである。
33 Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima; msiyapuuze.
教訓を聞いて、知恵を得よ、これを捨ててはならない。
34 Heri mtu yule anisikilizaye mimi, akisubiri siku zote malangoni mwangu, akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu.
わたしの言うことを聞き、日々わたしの門のかたわらでうかがい、わたしの戸口の柱のわきで待つ人はさいわいである。
35 Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana.
それは、わたしを得る者は命を得、主から恵みを得るからである。
36 Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”
わたしを失う者は自分の命をそこなう、すべてわたしを憎む者は死を愛する者である」。

< Mithali 8 >