< Mithali 8 >

1 Je, hekima haitani? Je, ufahamu hapazi sauti?
智慧豈不呼叫? 聰明豈不發聲?
2 Juu ya miinuko karibu na njia, penye njia panda, ndipo asimamapo;
她在道旁高處的頂上, 在十字路口站立,
3 kando ya malango yaelekeayo mjini, kwenye maingilio, hulia kwa sauti kubwa, akisema:
在城門旁,在城門口, 在城門洞,大聲說:
4 “Ni ninyi wanaume, ninaowaita; ninapaza sauti yangu kwa wanadamu wote.
眾人哪,我呼叫你們, 我向世人發聲。
5 Ninyi ambao ni wajinga, pateni akili; ninyi mlio wapumbavu, pateni ufahamu.
說:愚蒙人哪,你們要會悟靈明; 愚昧人哪,你們當心裏明白。
6 Sikilizeni, kwa maana nina mambo muhimu ya kusema; ninafungua midomo yangu kusema lililo sawa.
你們當聽,因我要說極美的話; 我張嘴要論正直的事。
7 Kinywa changu husema lililo kweli, kwa maana midomo yangu huchukia uovu.
我的口要發出真理; 我的嘴憎惡邪惡。
8 Maneno yote ya kinywa changu ni haki; hakuna mojawapo lililopotoka wala ukaidi.
我口中的言語都是公義, 並無彎曲乖僻。
9 Kwa wenye kupambanua yote ni sahihi; hayana kasoro kwa wale wenye maarifa.
有聰明的,以為明顯, 得知識的,以為正直。
10 Chagua mafundisho yangu badala ya fedha, maarifa badala ya dhahabu safi,
你們當受我的教訓,不受白銀; 寧得知識,勝過黃金。
11 kwa maana hekima ina thamani kuliko marijani na hakuna chochote unachohitaji kinacholingana naye.
因為智慧比珍珠更美; 一切可喜愛的都不足與比較。
12 “Mimi hekima, nakaa pamoja na busara; ninamiliki maarifa na busara.
我-智慧以靈明為居所, 又尋得知識和謀略。
13 Kumcha Bwana ni kuchukia uovu; ninachukia kiburi na majivuno, tabia mbaya na mazungumzo potovu.
敬畏耶和華在乎恨惡邪惡; 那驕傲、狂妄,並惡道, 以及乖謬的口,都為我所恨惡。
14 Ushauri na hukumu sahihi ni vyangu; nina ufahamu na nina nguvu.
我有謀略和真知識; 我乃聰明,我有能力。
15 Kwa msaada wangu wafalme hutawala na watawala hutunga sheria zilizo za haki,
帝王藉我坐國位; 君王藉我定公平。
16 kwa msaada wangu wakuu hutawala, na wenye vyeo wote watawalao dunia.
王子和首領, 世上一切的審判官,都是藉我掌權。
17 Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.
愛我的,我也愛他; 懇切尋求我的,必尋得見。
18 Utajiri na heshima viko kwangu, utajiri udumuo na mafanikio.
豐富尊榮在我; 恆久的財並公義也在我。
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu safi; kile nitoacho hupita fedha iliyo bora.
我的果實勝過黃金,強如精金; 我的出產超乎高銀。
20 Natembea katika njia ya unyofu katika mapito ya haki,
我在公義的道上走, 在公平的路中行,
21 nawapa utajiri wale wanipendao na kuzijaza hazina zao.
使愛我的,承受貨財, 並充滿他們的府庫。
22 “Bwana aliniumba mwanzoni mwa kazi yake, kabla ya matendo yake ya zamani;
在耶和華造化的起頭, 在太初創造萬物之先,就有了我。
23 niliteuliwa tangu milele, tangu mwanzoni, kabla ya dunia kuumbwa.
從亙古,從太初, 未有世界以前,我已被立。
24 Wakati hazijakuwepo bahari, nilikwishazaliwa, wakati hazijakuwepo chemchemi zilizojaa maji;
沒有深淵, 沒有大水的泉源,我已生出。
25 kabla milima haijawekwa mahali pake, kabla vilima havijakuwepo, nilikwishazaliwa,
大山未曾奠定, 小山未有之先,我已生出。
26 kabla hajaumba dunia wala mashamba yake au vumbi lolote la dunia.
耶和華還沒有創造大地和田野, 並世上的土質,我已生出。
27 Nilikuwepo alipoziweka mbingu mahali pake, wakati alichora mstari wa upeo wa macho juu ya uso wa kilindi,
他立高天,我在那裏; 他在淵面的周圍,劃出圓圈。
28 wakati aliweka mawingu juu na kuziweka imara chemchemi za bahari,
上使穹蒼堅硬, 下使淵源穩固,
29 wakati aliiwekea bahari mpaka wake ili maji yasivunje agizo lake, na wakati aliweka misingi ya dunia.
為滄海定出界限,使水不越過他的命令, 立定大地的根基。
30 Wakati huo nilikuwa fundi stadi kando yake. Nilijazwa na furaha siku baada ya siku, nikifurahi daima mbele zake,
那時,我在他那裏為工師, 日日為他所喜愛, 常常在他面前踴躍,
31 nikifurahi katika dunia yake yote nami nikiwafurahia wanadamu.
踴躍在他為人預備可住之地, 也喜悅住在世人之間。
32 “Basi sasa wanangu, nisikilizeni; heri wale wanaozishika njia zangu.
眾子啊,現在要聽從我, 因為謹守我道的,便為有福。
33 Sikilizeni mafundisho yangu mwe na hekima; msiyapuuze.
要聽教訓就得智慧, 不可棄絕。
34 Heri mtu yule anisikilizaye mimi, akisubiri siku zote malangoni mwangu, akingoja kwenye vizingiti vya mlango wangu.
聽從我、日日在我門口仰望、 在我門框旁邊等候的,那人便為有福。
35 Kwa maana yeyote anipataye mimi amepata uzima na kujipatia kibali kutoka kwa Bwana.
因為尋得我的,就尋得生命, 也必蒙耶和華的恩惠。
36 Lakini yeyote ashindwaye kunipata hujiumiza mwenyewe; na wote wanichukiao mimi hupenda mauti.”
得罪我的,卻害了自己的性命; 恨惡我的,都喜愛死亡。

< Mithali 8 >