< Mithali 7 >

1 Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
Hijo mío, guarda mis palabras Y atesora mis mandamientos dentro de ti.
2 Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
Guarda mis mandamientos y vive, Y mi enseñanza como la niña de tu ojo.
3 Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
Átalos a tus dedos. Escríbelos en la tabla de tu corazón.
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
Dí a la sabiduría: Tú eres mi hermana. Llama al entendimiento [tu] íntimo amigo,
5 watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
Para que te guarden de la mujer ajena, De la seductora [que] lisonjea con sus palabras.
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
Pues cuando desde la ventana de mi casa Observaba entre las celosías,
7 Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
Vi entre los ingenuos. Observé entre los jóvenes A un joven falto de entendimiento
8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
Que pasaba por la calle cerca de la esquina de ella. Caminaba en dirección a la casa de ella
9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
Al anochecer, cuando ya oscurecía, En medio de la noche y la oscuridad.
10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
Y ahí estaba una mujer que [salía] a encontrarlo, Astuta de corazón, vestida de prostituta,
11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
Bullanguera y desenfrenada. Sus pies no pueden permanecer en casa,
12 mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
Unas veces en las calles, otras en las plazas, Acecha en todas las esquinas.
13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
Lo agarró y lo besó, Y descaradamente le dijo:
14 “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
Prometí sacrificios de paz. Hoy pagué mis votos.
15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
Por tanto salí a encontrarte, A buscar diligentemente tu rostro, y te hallé.
16 Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
Preparé mi cama con colchas. La tendí con lino de Egipto.
17 Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
Perfumé mi cama con mirra, áloes, y canela.
18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
Ven, deleitémonos con caricias hasta el alba. Embriaguémonos de amores,
19 Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
Porque mi esposo no está en casa. Emprendió un largo viaje.
20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
Llevó consigo una bolsa de dinero. El día de luna nueva volverá a su casa.
21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
Lo rindió con la mucha suavidad de sus palabras. Lo sedujo con sus labios lisonjeros.
22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
Súbitamente se fue tras ella, Como el buey al matadero, Como un venado que se enredó en la trampa,
23 mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
Como ave que se lanza contra la red, Sin saber que le costará la vida, Hasta que una flecha le traspasa el hígado.
24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
Ahora pues, hijos, escúchenme. Presten atención a las palabras de mi boca:
25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
No dejes que tu corazón se aparte a los caminos de ella, Ni te extravíes por sus sendas.
26 Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
Porque ella dejó muchos heridos, Y aun los más fuertes fueron asesinados por ella.
27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
Su casa es el camino al Seol, Que desciende a las cámaras de la muerte. (Sheol h7585)

< Mithali 7 >