< Mithali 7 >

1 Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
Synu můj, ostříhej řečí mých, a přikázaní má schovej u sebe.
2 Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
Ostříhej přikázaní mých, a živ budeš, a naučení mého jako zřítelnice očí svých.
3 Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
Přivaž je na prsty své, napiš je na tabuli srdce svého.
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
Rci moudrosti: Sestra má jsi ty, a rozumnost přítelkyní jmenuj,
5 watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
Aby tě ostříhala od ženy cizí, od postranní, jenž řečmi svými lahodí.
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
Nebo z okna domu svého okénkem vyhlédaje,
7 Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
Viděl jsem mezi hloupými, spatřil jsem mezi mládeží mládence bláznivého.
8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
Kterýž šel po ulici vedlé úhlu jejího, a cestou k domu jejímu kráčel,
9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
V soumrak, u večer dne, ve tmách nočních a v mrákotě.
10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
A aj, žena potkala ho v ozdobě nevěstčí a chytrého srdce,
11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
Štěbetná a opovážlivá, v domě jejím nezůstávají nohy její,
12 mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
Jednak vně, jednak na ulici u každého úhlu úklady činící.
13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
I chopila jej, a políbila ho, a opovrhši stud, řekla jemu:
14 “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
Oběti pokojné jsou u mne, dnes splnila jsem slib svůj.
15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
Protož vyšla jsem vstříc tobě, abych pilně hledala tváři tvé, i nalezla jsem tě.
16 Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
Koberci jsem obestřela lůže své, s řezbami a prostěradly Egyptskými,
17 Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
Vykadila jsem pokojík svůj mirrou a aloe a skořicí.
18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
Poď, opojujme se milostí až do jitra, obveselíme se v milosti.
19 Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
Nebo není muže doma, odšel na cestu dalekou.
20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
Pytlík peněz vzal s sebou, v jistý den vrátí se do domu svého.
21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
I naklonila ho mnohými řečmi svými, a lahodností rtů svých přinutila jej.
22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
Šel za ní hned, jako vůl k zabití chodívá, a jako blázen v pouta, jimiž by trestán byl.
23 mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
Dokudž nepronikla střela jater jeho, pospíchal jako pták k osídlu, nevěda, že ono bezživotí jeho jest.
24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
Protož nyní, synové, slyšte mne, a pozorujte řečí úst mých.
25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
Neuchyluj se k cestám jejím srdce tvé, aniž se toulej po stezkách jejích.
26 Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
Nebo mnohé zranivši, porazila, a silní všickni zmordováni jsou od ní.
27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
Cesty pekelné dům její, vedoucí do skrýší smrti. (Sheol h7585)

< Mithali 7 >