< Mithali 7 >
1 Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
Synu můj, ostříhej řečí mých, a přikázaní má schovej u sebe.
2 Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
Ostříhej přikázaní mých, a živ budeš, a naučení mého jako zřítelnice očí svých.
3 Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
Přivaž je na prsty své, napiš je na tabuli srdce svého.
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
Rci moudrosti: Sestra má jsi ty, a rozumnost přítelkyní jmenuj,
5 watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
Aby tě ostříhala od ženy cizí, od postranní, jenž řečmi svými lahodí.
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
Nebo z okna domu svého okénkem vyhlédaje,
7 Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
Viděl jsem mezi hloupými, spatřil jsem mezi mládeží mládence bláznivého.
8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
Kterýž šel po ulici vedlé úhlu jejího, a cestou k domu jejímu kráčel,
9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
V soumrak, u večer dne, ve tmách nočních a v mrákotě.
10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
A aj, žena potkala ho v ozdobě nevěstčí a chytrého srdce,
11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
Štěbetná a opovážlivá, v domě jejím nezůstávají nohy její,
12 mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
Jednak vně, jednak na ulici u každého úhlu úklady činící.
13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
I chopila jej, a políbila ho, a opovrhši stud, řekla jemu:
14 “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
Oběti pokojné jsou u mne, dnes splnila jsem slib svůj.
15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
Protož vyšla jsem vstříc tobě, abych pilně hledala tváři tvé, i nalezla jsem tě.
16 Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
Koberci jsem obestřela lůže své, s řezbami a prostěradly Egyptskými,
17 Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
Vykadila jsem pokojík svůj mirrou a aloe a skořicí.
18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
Poď, opojujme se milostí až do jitra, obveselíme se v milosti.
19 Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
Nebo není muže doma, odšel na cestu dalekou.
20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
Pytlík peněz vzal s sebou, v jistý den vrátí se do domu svého.
21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
I naklonila ho mnohými řečmi svými, a lahodností rtů svých přinutila jej.
22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
Šel za ní hned, jako vůl k zabití chodívá, a jako blázen v pouta, jimiž by trestán byl.
23 mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
Dokudž nepronikla střela jater jeho, pospíchal jako pták k osídlu, nevěda, že ono bezživotí jeho jest.
24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
Protož nyní, synové, slyšte mne, a pozorujte řečí úst mých.
25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
Neuchyluj se k cestám jejím srdce tvé, aniž se toulej po stezkách jejích.
26 Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
Nebo mnohé zranivši, porazila, a silní všickni zmordováni jsou od ní.
27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol )
Cesty pekelné dům její, vedoucí do skrýší smrti. (Sheol )