< Mithali 7 >

1 Mwanangu, shika maneno yangu na kuzihifadhi amri zangu ndani yako.
我兒,你要持守我的訓言,把我的誡命藏在心中;
2 Shika amri zangu nawe utaishi; linda mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.
你要遵守我的誡命,好叫你得以生存;應恪守我的教訓,像保護你眼中的瞳人。
3 Yafunge katika vidole vyako; yaandike katika kibao cha moyo wako.
應將我的誡命繫在指間,刻在心上;
4 Mwambie hekima, “Wewe ni dada yangu,” uite ufahamu jamaa yako;
應對智慧說:「你是我的姊妹,」並應稱睿智為你的女友,
5 watakuepusha na mwanamke mzinzi, kutokana na mwanamke mpotovu na maneno yake ya kubembeleza.
好能保護你遠避奸婦,即那甜言蜜語的淫婦。
6 Kwenye dirisha la nyumba yangu nilitazama nje kupitia upenyo kwenye mwimo wa dirisha.
我曾由我家的窗口,透過窗格往外觀看,
7 Niliona miongoni mwa wajinga, nikagundua miongoni mwa wanaume vijana, kijana asiye na akili.
分明看見在愚昧人中,在少年人中,有一個無知的少年,
8 Alikuwa akishuka njiani karibu na pembe ya kwake, akielekea kwenye nyumba ya huyo mwanamke
沿著淫婦屋角的街道經過,向她的住宅走去,
9 wakati wa machweo, jua likipungua nuru yake, giza la usiku lilipokuwa likiingia.
那時正是黃昏,日已西沉,已入黝黑深夜。
10 Ndipo huyo mwanamke akatoka kumlaki, hali amevaa kama kahaba akiwa na nia ya udanganyifu.
看,有一個女人向他迎面而來──她身穿妓裝,存心不軌;
11 (Ni mwanamke mwenye makelele na mkaidi, miguu yake haitulii nyumbani;
她健談好蕩,不能停留家中:
12 mara kwenye barabara za mji, mara kwenye viwanja vikubwa, kwenye kila pembe huvizia.)
一會在街頭,一會在市場,在每個角落上兜搭──
13 Huyo mwanamke alimkumbatia kijana na kumbusu, na kwa uso usio na haya akamwambia:
她遂上前擁抱那少年,與他接吻,嬉皮笑臉對他說:「
14 “Nina sadaka za amani nyumbani; leo nimetimiza nadhiri zangu.
我原許過願,要獻和平祭,今日纔得償還我許的願。
15 Kwa hiyo nimetoka nje kukulaki; nimekutafuta na nimekupata!
所以我走了出來,好能與你相遇;我急切尋找你,可好現在我見了你。
16 Nimetandika kitanda changu kwa kitani za rangi kutoka Misri.
我的床榻已舖設了絨毯,放上了埃及的線繡臥單;
17 Nimetia manukato kitanda changu kwa manemane, udi na mdalasini.
又用沒藥、蘆薈和肉桂薰了我的睡床。
18 Njoo, tuzame katika mapenzi mpaka asubuhi; tujifurahishe wenyewe kwa mapenzi!
來讓我們通宵達旦,飽享愛情;讓我們在歡愛中盡情取樂,
19 Mume wangu hayupo nyumbani; amekwenda safari ya mbali.
因為我的丈夫現不在家,他已出外遠行,
20 Amechukua mkoba uliojazwa fedha na hatakuwepo nyumbani karibuni.”
隨身帶了錢囊,不到月圓不歸家。」
21 Kwa maneno laini yule mwanamke akampotosha; alimshawishi kwa maneno yake laini.
淫婦用許多花言巧語籠絡他,以諂言媚語勾引他。
22 Mara huyo kijana alimfuata yule mwanamke kama fahali aendaye machinjoni, kama kulungu aingiaye kwenye kitanzi,
少年遂跟她去了,好像一隻引入屠場的公牛,又像一隻自陷圈套的牡鹿,
23 mpaka mshale umchome ini lake, kama ndege anayenaswa kwenye mtego, bila kujua itamgharimu maisha yake.
直至箭矢射穿他的心肝;他還像一隻跳入羅網的小鳥,不知這與他的性命有關。
24 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; sikilizeni kwa makini nisemalo.
現在,孩子! 你們應聽從我,留意我口中的訓言:
25 Usiruhusu moyo wako ugeukie njia za huyo mwanamke, wala usitangetange katika mapito yake.
不要讓你的心傾向她的道路,不要誤入她的迷途,
26 Aliowaangusha ni wengi; aliowachinja ni kundi kubwa.
因為她使許多人倒地身亡,連最強健的,都作了她的犧牲。
27 Nyumba yake ni njia kuu iendayo kaburini, ielekeayo chini kwenye vyumba vya mauti. (Sheol h7585)
她的家是通往陰府的大道,是引入死境的斜坡。 (Sheol h7585)

< Mithali 7 >