< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
HIJO mío, si salieres fiador por tu amigo, si tocaste tu mano por el extraño,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
Enlazado eres con las palabras de tu boca, y preso con las razones de tu boca.
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Haz esto ahora, hijo mío, y líbrate, ya que has caído en la mano de tu prójimo: ve, humíllate, y asegúrate de tu amigo.
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
No des sueño á tus ojos, ni á tus párpados adormecimiento.
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Escápate como el corzo de la mano [del cazador], y como el ave de la mano del parancero.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Ve á la hormiga, oh perezoso, mira sus caminos, y sé sabio;
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
La cual no teniendo capitán, ni gobernador, ni señor,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Prepara en el verano su comida y allega en el tiempo de la siega su mantenimiento.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Perezoso, ¿hasta cuándo has de dormir? ¿cuándo te levantarás de tu sueño?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Un poco de sueño, un poco de dormitar, y cruzar por un poco las manos para reposo:
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Así vendrá tu necesidad como caminante, y tu pobreza como hombre de escudo.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
El hombre malo, el hombre depravado, anda en perversidad de boca;
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
Guiña de sus ojos, habla con sus pies, indica con sus dedos;
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
Perversidades hay en su corazón, anda pensando mal en todo tiempo; enciende rencillas.
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
Por tanto su calamidad vendrá de repente; súbitamente será quebrantado, y no [habrá] remedio.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Seis cosas aborrece Jehová, y aun siete abomina su alma:
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Los ojos altivos, la lengua mentirosa, las manos derramadoras de sangre inocente,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
El corazón que maquina pensamientos inicuos, los pies presurosos para correr al mal,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
El testigo falso que habla mentiras, y el que enciende rencillas entre los hermanos.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Guarda, hijo mío, el mandamiento de tu padre, y no dejes la enseñanza de tu madre:
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
Atalos siempre en tu corazón, enlázalos á tu cuello.
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
Te guiarán cuando anduvieres; cuando durmieres te guardarán; hablarán contigo cuando despertares.
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
Porque el mandamiento es antorcha, y la enseñanza luz; y camino de vida las reprensiones de la enseñanza:
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
Para que te guarden de la mala mujer, de la blandura de la lengua de la extraña.
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
No codicies su hermosura en tu corazón, ni ella te prenda con sus ojos:
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Porque á causa de la mujer ramera [es reducido el hombre] á un bocado de pan; y la mujer caza la preciosa alma del varón.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
¿Tomará el hombre fuego en su seno, sin que sus vestidos se quemen?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
¿Andará el hombre sobre las brasas, sin que sus pies se abrasen?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Así el que entrare á la mujer de su prójimo; no será sin culpa cualquiera que la tocare.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
No tienen en poco al ladrón, cuando hurtare para saciar su alma teniendo hambre:
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Empero tomado, paga las setenas, da toda la sustancia de su casa.
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Mas el que comete adulterio con la mujer, es falto de entendimiento: corrompe su alma el que tal hace.
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
Plaga y vergüenza hallará; y su afrenta nunca será raída.
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Porque los celos son el furor del hombre, y no perdonará en el día de la venganza.
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
No tendrá respeto á ninguna redención; ni querrá [perdonar], aunque multipliques los dones.

< Mithali 6 >