< Mithali 6 >
1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
Hijo mío, si saliste fiador por tu prójimo, Si empeñaste tu palabra a un extraño,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
Si te enredaste con tus palabras, Y quedaste atrapado con los dichos de tu boca,
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Haz esto ahora, hijo mío, y líbrate. Ya que caíste en las manos de tu prójimo: Vé, humíllate e importuna a tu prójimo.
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
No concedas sueño a tus ojos, Ni adormecimiento a tus párpados.
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Líbrate como gacela de la mano [del cazador], Como un ave de la trampa.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Mira a la hormiga, oh perezoso, Observa sus caminos y sé sabio,
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
La cual, sin tener jefe, Ni gobernador, ni soberano,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Prepara en el verano su comida. En el tiempo de la cosecha guarda su sustento.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
¿Hasta cuándo estarás acostado, oh perezoso? ¿Cuándo te levantarás de tu sueño?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Un rato duermes, otro dormitas, Un rato cruzas los brazos y descansas.
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Te llega la miseria como un vagabundo, Y tu necesidad como un hombre armado.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
Hombre depravado es el hombre inicuo, Que anda en la perversidad de su boca,
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
Guiña con un ojo, menea los pies, Hace señas con los dedos.
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
En su corazón hay perversidades, Maquina maldades, y continuamente busca rencillas.
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
Por tanto, su calamidad vendrá de repente. Súbitamente será quebrantado y no habrá remedio.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Seis [cosas] aborrece Yavé, Y aun siete repugna su alma:
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Ojos altivos, boca mentirosa, Manos que derraman sangre inocente,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
Corazón que maquina planes perversos, Pies presurosos para correr al mal,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Testigo falso que habla mentiras, Y el que enciende discordias entre sus hermanos.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Hijo mío, guarda el mandamiento de tu padre, Y no abandones la instrucción de tu madre.
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
Átalos continuamente a tu corazón, Enlázalos en torno a tu cuello.
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
Cuando camines, te guiarán. Cuando duermas, te protegerán. Hablarán contigo al despertar.
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
Porque el mandamiento es lámpara, La enseñanza es luz Y camino de vida las reprensiones de la instrucción.
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
Te guardarán de la mala mujer, De la blandura de la boca de la mujer extraña.
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
No codicies en tu corazón su hermosura, Ni dejes que te cautive con sus párpados.
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Porque si la prostituta busca una hogaza de pan, La adúltera caza una vida preciosa.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
¿Tomará el hombre fuego en su seno, Sin que ardan sus ropas?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
¿Andará un hombre sobre brasas, Sin que se quemen sus pies?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Así sucederá con el que se une a la mujer de su prójimo. Ninguno que la toque quedará impune.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
¿No desprecian al ladrón aunque robe Para llenar su estómago cuando tiene hambre?
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Si es sorprendido, tiene que pagar siete veces Y entregar todo lo que tiene en su casa.
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Pues el adúltero es hombre sin cordura, Destructor de sí mismo es el que lo hace.
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
Heridas y deshonra hallará, Y su afrenta no será borrada.
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Porque los celos son la ira del hombre. En el día de la venganza no perdonará,
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
Ni aceptará algún rescate. No se aplacará aunque ofrezcas muchos regalos.