< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
わが子よ、あなたがもし隣り人のために保証人となり、他人のために手をうって誓ったならば、
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
もしあなたのくちびるの言葉によって、わなにかかり、あなたの口の言葉によって捕えられたならば、
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
わが子よ、その時はこうして、おのれを救え、あなたは隣り人の手に陥ったのだから。急いで行って、隣り人にひたすら求めよ。
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
あなたの目を眠らせず、あなたのまぶたを、まどろませず、
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
かもしかが、かりゅうどの手からのがれるように、鳥が鳥を取る者の手からのがれるように、おのれを救え。
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
なまけ者よ、ありのところへ行き、そのすることを見て、知恵を得よ。
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
ありは、かしらなく、つかさなく、王もないが、
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
夏のうちに食物をそなえ、刈入れの時に、かてを集める。
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
なまけ者よ、いつまで寝ているのか、いつ目をさまして起きるのか。
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
しばらく眠り、しばらくまどろみ、手をこまぬいて、またしばらく休む。
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
それゆえ、貧しさは盗びとのようにあなたに来り、乏しさは、つわもののようにあなたに来る。
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
よこしまな人、悪しき人は偽りの言葉をもって行きめぐり、
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
目でめくばせし、足で踏み鳴らし、指で示し、
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
よこしまな心をもって悪を計り、絶えず争いをおこす。
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
それゆえ、災は、にわかに彼に臨み、たちまちにして打ち敗られ、助かることはない。
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
主の憎まれるものが六つある、否、その心に、忌みきらわれるものが七つある。
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
すなわち、高ぶる目、偽りを言う舌、罪なき人の血を流す手、
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
悪しき計りごとをめぐらす心、すみやかに悪に走る足、
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
偽りをのべる証人、また兄弟のうちに争いをおこす人がこれである。
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
わが子よ、あなたの父の戒めを守り、あなたの母の教を捨てるな。
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
つねに、これをあなたの心に結び、あなたの首のまわりにつけよ。
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
これは、あなたが歩くとき、あなたを導き、あなたが寝るとき、あなたを守り、あなたが目ざめるとき、あなたと語る。
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
戒めはともしびである、教は光である、教訓の懲しめは命の道である。
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
これは、あなたを守って、悪い女に近づかせず、みだらな女の、巧みな舌に惑わされぬようにする。
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
彼女の麗しさを心に慕ってはならない、そのまぶたに捕えられてはならない。
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
遊女は一塊のパンのために雇われる、しかし、みだらな女は人の尊い命を求める。
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
人は火を、そのふところにいだいてその着物が焼かれないであろうか。
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
また人は、熱い火を踏んで、その足が、焼かれないであろうか。
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
その隣の妻と不義を行う者も、それと同じだ。すべて彼女に触れる者は罰を免れることはできない。
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
盗びとが飢えたとき、その飢えを満たすために盗むならば、人は彼を軽んじないであろうか。
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
もし捕えられたなら、その七倍を償い、その家の貨財を、ことごとく出さなければならない。
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
女と姦淫を行う者は思慮がない。これを行う者はおのれを滅ぼし、
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
傷と、はずかしめとを受けて、その恥をすすぐことができない。
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
ねたみは、その夫を激しく怒らせるゆえ、恨みを報いるとき、容赦することはない。
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
どのようなあがない物をも顧みず、多くの贈り物をしても、和らがない。

< Mithali 6 >