< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
我子よ汝もし朋友のために保證をなし 他人のために汝の手を拍ば
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
汝その口の言によりてわなにかかり その口の言によりてとらへらるるなり
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
我子よ汝友の手に陷りしならば斯して自ら救へ すなはち往て自ら謙だり只管なんぢの友に求め
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
汝の目をして睡らしむることなく 汝の眼瞼をして閉しむること勿れ
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
かりうどの手より鹿ののがるるごとく 鳥とる者の手より鳥ののがるる如くして みづからを救へ
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
惰者よ蟻にゆき其爲すところを觀て智慧をえよ
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
蟻は首領なく有司なく君主なけれども
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
夏のうちに食をそなへ 収穫のときに糧を斂む
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
惰者よ汝いづれの時まで臥息むや いづれの時まで睡りて起ざるや
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
しばらく臥ししばらく睡り 手を叉きてまた片時やすむ
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
さらば汝の貧窮は盗人の如くきたり汝の缺乏は兵士の如くきたるべし
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
邪曲なる人あしき人は虚偽の言をもて事を行ふ
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
彼は眼をもて眴せし 脚をもてしらせ 指をもて示す
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
その心に虚偽をたもち 常に惡をはかり 爭端を起す
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
この故にその禍害にはかに來り 援助なくして立刻に敗らるべし
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
ヱホバの憎みたまふもの六あり 否その心に嫌ひたまふもの七あり
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
即ち驕る目いつはりをいふ舌 つみなき人の血を流す手
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
惡き謀計をめぐらす心 すみやかに惡に趨る足
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
詐僞をのぶる證人 および兄弟のうちに爭端をおこす者なり
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
我子よ汝の父の誡命を守り 汝の母の法を棄る勿れ
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
常にこれを汝の心にむす び之をなんぢの頸に佩よ
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
これは汝のゆくとき汝をみちびき 汝の寝るとき汝をまもり 汝の寤るとき汝とかたらん
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
それ誡命は燈火なり 法は光なり 敎訓の懲治は生命の道なり
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
これは汝をまもりて惡き婦よりまぬかれしめ 汝をたもちて淫婦の舌の諂媚にまどはされざらしめん
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
その艶美を心に戀ふことなかれ その眼瞼に捕へらるること勿れ
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
それ娼妓のために人はただ僅に一撮の糧をのこすのみにいたる 又淫婦は人の尊き生命を求むるなり
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
人は火を懐に抱きてその衣を焚れざらんや
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
人は熱火を踏て其足を焚れざらんや
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
その隣の妻と姦淫をおこなふ者もかくあるべし 凡て之に捫る者は罪なしとせられず
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
竊む者もし饑しときに其饑を充さん爲にぬすめるならば人これを藐ぜじ
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
もし捕へられなばその七倍を償ひ其家の所有をことごとく出さざるべからず
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
婦と姦淫をおこなふ者は智慧なきなり 之を行ふ者はおのれの霊魂を亡し
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
傷と陵辱とをうけて其恥を雪ぐこと能はず
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
妒忌その夫をして忿怒をもやさしむればその怨を報ゆるときかならず寛さじ
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
いかなる贖物をも顧みず 衆多の饋物をなすともやはらがざるべし

< Mithali 6 >