< Mithali 6 >
1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
Mon fils, si tu as cautionné ton prochain, si tu as répondu pour quelqu'un,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
Tu es enlacé par les paroles de ta bouche; tu es pris par les paroles de ta bouche.
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Mon fils, fais promptement ceci: dégage-toi; puisque tu es tombé entre les mains de ton prochain, va, prosterne-toi, et supplie ton prochain.
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
Ne donne point de sommeil à tes yeux, ni de repos à tes paupières;
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Dégage-toi comme le daim de la main du chasseur, et comme l'oiseau de la main de l'oiseleur.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Paresseux, va vers la fourmi, regarde ses voies, et deviens sage.
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
Elle n'a ni chef, ni surveillant, ni maître,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Elle prépare sa nourriture en été, et amasse durant la moisson de quoi manger.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Paresseux, jusques à quand seras-tu couché? Quand te lèveras-tu de ton sommeil?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Un peu dormir, un peu sommeiller, un peu croiser les mains pour se reposer;
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Et la pauvreté viendra comme un coureur, et la disette comme un homme armé.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
Le méchant homme, l'homme inique va avec une bouche perverse.
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
Il fait signe de ses yeux, il parle de ses pieds, il donne à entendre de ses doigts.
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
La perversité est dans son cœur, il machine du mal en tout temps, il fait naître des querelles.
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
C'est pourquoi sa ruine viendra tout d'un coup; il sera subitement brisé, il n'y aura point de guérison.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Il y a six choses que hait l'Éternel, même sept qui lui sont en abomination:
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Les yeux hautains, la langue fausse, les mains qui répandent le sang innocent,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
Le cœur qui forme de mauvais desseins, les pieds qui se hâtent pour courir au mal,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Le faux témoin qui prononce des mensonges, et celui qui sème des querelles entre les frères.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Mon fils, garde le commandement de ton père, et n'abandonne point l'enseignement de ta mère.
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
Tiens-les continuellement liés sur ton cœur, et les attache à ton cou.
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
Quand tu marcheras, ils te conduiront; quand tu te coucheras, ils te garderont; quand tu te réveilleras, ils te parleront.
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
Car le commandement est une lampe, l'enseignement est une lumière, et les corrections propres à instruire sont le chemin de la vie.
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
Pour te garder de la femme corrompue, et de la langue flatteuse d'une étrangère,
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
Ne convoite point sa beauté dans ton cœur, et ne te laisse pas prendre par ses yeux.
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Car pour l'amour de la femme débauchée on est réduit à un morceau de pain, et la femme adultère chasse après l'âme précieuse de l'homme.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
Quelqu'un peut-il prendre du feu dans son sein, sans que ses habits brûlent?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
Quelqu'un marchera-t-il sur la braise, sans que ses pieds soient brûlés?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Il en est de même pour celui qui entre vers la femme de son prochain; quiconque la touchera ne sera point impuni.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
On ne laisse pas impuni le voleur qui ne dérobe que pour se rassasier, quand il a faim;
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Et s'il est surpris, il rendra sept fois autant, il donnera tout ce qu'il a dans sa maison.
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Mais celui qui commet adultère avec une femme, est dépourvu de sens; celui qui veut se perdre fera cela.
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
Il trouvera des plaies et de l'ignominie, et son opprobre ne sera point effacé;
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Car la jalousie du mari est une fureur, et il sera sans pitié au jour de la vengeance.
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
Il n'aura égard à aucune rançon, et n'acceptera rien, quand même tu multiplierais les présents.