< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
Mia filo! se vi garantiis por via proksimulo Kaj donis vian manon por aliulo,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
Tiam vi enretiĝis per la vortoj de via buŝo, Kaptiĝis per la vortoj de via buŝo.
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Tiam, mia filo, agu tiel kaj saviĝu, Ĉar vi falis en la mano de via proksimulo: Iru, vigliĝu, kaj petegu vian proksimulon;
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
Ne lasu viajn okulojn dormi Kaj viajn palpebrojn dormeti;
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Savu vin, kiel gazelo, el la mano, Kaj kiel birdo el la mano de la birdokaptisto.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Iru al la formiko, vi maldiligentulo; Rigardu ĝian agadon, kaj saĝiĝu.
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
Kvankam ĝi ne havas estron, Nek kontrolanton, nek reganton,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Ĝi pretigas en la somero sian panon, Ĝi kolektas dum la rikolto sian manĝon.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Ĝis kiam, maldiligentulo, vi kuŝos? Kiam vi leviĝos de via dormo?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Iom da dormo, iom da dormeto, Iom da kunmeto de la manoj por kuŝado;
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Kaj venos via malriĉeco kiel rabisto, Kaj via senhaveco kiel viro armita.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
Homo sentaŭga, homo malbonfarema, Iras kun buŝo malica,
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
Donas signojn per la okuloj, aludas per siaj piedoj, Komprenigas per siaj fingroj;
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
Perverseco estas en lia koro, li intencas malbonon; En ĉiu tempo li semas malpacon.
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
Tial subite venos lia pereo; Li estos rompita subite, kaj neniu lin sanigos.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Jen estas ses aferoj, kiujn la Eternulo malamas, Kaj sep, kiujn Li abomenegas.
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Arogantaj okuloj, mensogema lango, Kaj manoj, kiuj verŝas senkulpan sangon,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
Koro, kiu preparas malbonfarajn intencojn, Piedoj, kiuj rapidas kuri al malbono,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Falsa atestanto, kiu elspiras mensogojn; Kaj tiu, kiu semas malpacon inter fratoj.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Konservu, mia filo, la ordonon de via patro, Kaj ne forĵetu la instruon de via patrino.
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
Ligu ilin por ĉiam al via koro, Volvu ilin sur vian kolon.
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
Kiam vi iros, ili gvidos vin; Kiam vi kuŝiĝos, ili vin gardos; Kaj kiam vi vekiĝos, ili parolos kun vi.
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
Ĉar moralordono estas lumingo, kaj instruo estas lumo, Kaj edifaj predikoj estas vojo de vivo,
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
Por gardi vin kontraŭ malbona virino, Kontraŭ glata lango de fremdulino.
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
Ne deziregu en via koro ŝian belecon, Kaj ne kaptiĝu per ŝiaj palpebroj.
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Ĉar la kosto de publikulino estas nur unu pano; Sed fremda edzino forkaptas la grandvaloran animon.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
Ĉu iu povas teni fajron en sia sino tiel, Ke liaj vestoj ne brulu?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
Ĉu iu povas marŝi sur ardantaj karboj, Ne bruligante siajn piedojn?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Tiel ankaŭ estas kun tiu, kiu venas al la edzino de sia proksimulo; Neniu, kiu ŝin ektuŝas, restas sen puno.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
Oni ne faras grandan honton al ŝtelanto, Se li ŝtelas por sin satigi, kiam li malsatas;
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Kaj kiam oni lin kaptas, li pagas sepoble; La tutan havon de sia domo li fordonas.
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Sed kiu adultas kun virino, tiu estas sensaĝa; Tiu, kiu faras tion, pereigas sian animon;
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
Batojn kaj malhonoron li ricevas, Kaj lia honto ne elviŝiĝas;
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Ĉar furiozas la ĵaluzo de la edzo; Kaj li ne indulgas en la tempo de la venĝo.
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
Li rigardas nenian kompenson, Kaj li ne akceptas, se vi volas eĉ multe donaci.

< Mithali 6 >