< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
Min Søn: har du borget for din næste og givet en anden Håndslag,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
er du fanget ved dine Læber og bundet ved Mundens Ord,
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
gør så dette, min Søn, og red dig, nu du er kommet i Næstens Hånd: Gå hen uden Tøven, træng ind på din Næste;
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
und ikke dine Øjne Søvn, ej heller dine Øjenlåg Hvile,
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
red dig som en Gazel af Snaren, som en Fugl af Fuglefængerens Hånd.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Gå hen til Myren, du lade, se dens Færd og bliv viis.
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
Skønt uden Fyrste, Foged og Styrer,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
sørger den dog om Somren for Æde og sanker sin Føde i Høst.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Hvor længe vil du ligge, du lade, når står du op af din Søvn?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Lidt Søvn endnu, lidt Blund, lidt Hvile med samlagte Hænder:
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
som en Stimand kommer da Fattigdom over dig, Trang som en skjoldvæbnet Mand.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
En Nidding, en ussel Mand er den, som vandrer med Falskhed i Munden,
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
som blinker med Øjet, skraber med Foden og giver Tegn med Fingrene,
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
som smeder Rænker i Hjertet og altid kun ypper Kiv;
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
derfor kommer hans Undergang brat, han knuses på Stedet, kan ikke læges.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Seks Ting hader HERREN, syv er hans Sjæl en Gru:
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Stolte Øjne, Løgnetunge, Hænder, der udgyder uskyldigt Blod,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
et Hjerte, der udtænker onde Råd, Fødder, der haster og iler til ondt,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
falsk Vidne, der farer med Løgn, og den, som sætter Splid mellem Brødre.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Min Søn, tag Vare på din Faders Bud, opgiv ikke din Moders Belæring,
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
bind dem altid på dit Hjerte, knyt dem fast om din Hals;
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
på din Vandring lede den dig, på dit Leje vogte den dig, den tale dig til, når du vågner;
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
thi Budet er en Lygte, Læren Lys, og Tugtens Revselse Livets Vej
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
for at vogte dig for Andenmands Hustru, for fremmed Kvindes sleske Tunge!
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
Attrå ej i dit Hjerte hendes Skønhed, hendes Blik besnære dig ej!
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Thi en Skøge får man blot for et Brød, men Andenmands Hustru fanger dyrebar Sjæl.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
Kan nogen bære Ild i sin Brystfold, uden at Klæderne brænder?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
Kan man vandre på glødende Kul, uden at Fødderne svides?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Så er det at gå ind til sin Næstes Hustru; ingen, der rører hende, slipper for Straf.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
Ringeagter man ikke Tyven, når han stjæler fot at stille sin Sult?
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Om han gribes, må han syvfold bøde og afgive alt sit Huses Gods.
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Afsindig er den, der boler med hende, kun en Selvmorder handler så;
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
han opnår Hug og Skændsel, og aldrig udslettes hans Skam.
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Thi Skinsyge vækker Mandens Vrede, han skåner ikke på Hævnens Dag;
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
ingen Bøde tager han god; store Tilbud rører ham ikke.

< Mithali 6 >