< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
Synu můj, slíbil-lis za přítele svého, podal-lis cizímu ruky své,
2 kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
Zapleten jsi slovy úst svých, jat jsi řečmi úst svých.
3 basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
Učiniž tedy toto, synu můj, a vyprosť se, poněvadžs se dostal v ruku přítele svého. Jdi, pokoř se, a probuď přítele svého.
4 Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
Nedej usnouti očím svým, a zdřímati víčkám svým.
5 Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Vydři se jako srna z ruky, a jako pták z ruky čižebníka.
6 Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
Jdi k mravenci, lenochu, shlédni cesty jeho, a nabuď moudrosti.
7 Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
Kterýž nemaje vůdce, ani správce, ani pána,
8 lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
Připravuje v létě pokrm svůj, shromažďuje ve žni potravu svou.
9 Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
Dokudž lenochu ležeti budeš? Skoro-liž vstaneš ze sna svého?
10 Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
Maličko pospíš, maličko zdřímeš, maličko složíš ruce, abys poležel,
11 hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
V tom přijde jako pocestný chudoba tvá, a nouze tvá jako muž zbrojný.
12 Mtu mbaya sana na mlaghai, ambaye huzungukazunguka na maneno ya upotovu,
Člověk nešlechetný, muž nepravý chodí v převrácenosti úst.
13 ambaye anakonyeza kwa jicho lake, anayetoa ishara kwa miguu yake na kuashiria kwa vidole vyake,
Mhourá očima svýma, mluví nohama svýma, ukazuje prsty svými.
14 ambaye hupanga ubaya kwa udanganyifu moyoni mwake: daima huchochea fitina.
Převrácenost všeliká jest v srdci jeho, smýšlí zlé všelikého času, sváry rozsívá.
15 Kwa hiyo maafa yatamkumba ghafula; ataangamizwa mara, pasipo msaada.
A protož v náhle přijde bída jeho, rychle setřín bude, a nebudeť uléčení.
16 Kuna vitu sita anavyovichukia Bwana, naam, viko saba vilivyo chukizo kwake:
Těchto šesti věcí nenávidí Hospodin, a sedmá ohavností jest duši jeho:
17 macho ya kiburi, ulimi udanganyao, mikono imwagayo damu isiyo na hatia,
Očí vysokých, jazyka lživého, a rukou vylévajících krev nevinnou,
18 moyo uwazao mipango miovu, miguu iliyo myepesi kukimbilia uovu,
Srdce, kteréž ukládá myšlení nepravá, noh kvapných běžeti ke zlému,
19 shahidi wa uongo ambaye humwaga uongo, na mtu ambaye huchochea fitina kati ya ndugu.
Svědka lživého, mluvícího lež, a toho, jenž rozsívá různice mezi bratřími.
20 Mwanangu, zishike amri za baba yako, wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Ostříhejž, synu můj, přikázaní otce svého, a neopouštěj naučení matky své.
21 Yafunge katika moyo wako daima, yakaze kuizunguka shingo yako.
Přivazuj je k srdci svému ustavičně, a k hrdlu svému je připínej.
22 Wakati utembeapo, yatakuongoza; wakati ulalapo, yatakulinda; wakati uamkapo, yatazungumza nawe.
Kamžkoli půjdeš, ono tě zprovodí, když spáti budeš, bude tě ostříhati, a když procítíš, bude s tebou rozmlouvati,
23 Kwa maana amri hizi ni taa, mafundisho haya ni mwanga na maonyo ya maadili ni njia ya uzima,
(Nebo přikázaní jest svíce, a naučení světlo, a cesta života jsou domlouvání vyučující),
24 yakikulinda na mwanamke aliyepotoka, kutokana na maneno laini ya mwanamke aliyepotoka.
Aby tě ostříhalo od ženy zlé, od úlisnosti jazyka ženy cizí.
25 Moyo wako usitamani uzuri wake wala macho yake yasikuteke,
Nežádejž krásy její v srdci svém, a nechať tě nejímá víčky svými.
26 kwa maana kahaba atakufanya uwe maskini, hata ukose kipande cha mkate, naye mwanamke mzinzi huwinda maisha yako hasa.
Nebo příčinou ženy cizoložné zchudl bys až do kusu chleba, anobrž žena cizoložná drahou duši ulovuje.
27 Je, mtu aweza kuchotea moto kwenye paja lake bila nguo zake kuungua?
Může-liž kdo skrýti oheň v klíně svém, aby roucho jeho se nepropálilo?
28 Je, mtu aweza kutembea juu ya makaa ya moto yanayowaka bila miguu yake kuungua?
Může-liž kdo choditi po uhlí řeřavém, aby nohy jeho se neopálily?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa mwanaume mwingine; hakuna yeyote amgusaye huyo mwanamke ambaye hataadhibiwa.
Tak kdož vchází k ženě bližního svého, nebudeť bez viny, kdož by se jí koli dotkl.
30 Watu hawamdharau mwizi kama akiiba kukidhi njaa yake wakati ana njaa.
Neuvozují potupy na zloděje, jestliže by ukradl, aby nasytil život svůj, když lační,
31 Pamoja na hayo, kama akikamatwa, lazima alipe mara saba, ingawa inamgharimu utajiri wote wa nyumba yake.
Ač postižen jsa, navracuje to sedmernásobně, vším statkem domu svého nahražuje:
32 Lakini mwanaume aziniye na mwanamke hana akili kabisa; yeyote afanyaye hivyo hujiangamiza mwenyewe.
Ale cizoložící s ženou blázen jest; kdož hubí duši svou, tenť to činí;
33 Mapigo na aibu ni fungu lake na aibu yake haitafutika kamwe;
Trápení a lehkosti dochází, a útržka jeho nebývá shlazena.
34 kwa maana wivu huamsha ghadhabu ya mume, naye hataonyesha huruma alipizapo kisasi.
Nebo zůřivý jest hněv muže, a neodpouštíť v den pomsty.
35 Hatakubali fidia yoyote; atakataa malipo, hata yakiwa makubwa kiasi gani.
Neohlídá se na žádnou záplatu, aniž přijímá, by i množství darů dával.

< Mithali 6 >