< Mithali 5 >
1 Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu, sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,
Hijo mío, presta atención a mi sabiduría, inclina tu oído a mi enseñanza,
2 ili uweze kutunza busara na midomo yako ihifadhi maarifa.
para que guardes los consejos y tus labios conserven la instrucción.
3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
Pues los labios de la mujer extraña destilan miel, y su paladar es más suave que el aceite;
4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.
pero su fin es amargo como el ajenjo, cortante como espada de dos filos.
5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini. (Sheol )
Sus pies se encaminan hacia la muerte, sus pasos llevan al scheol. (Sheol )
6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
No anda por la senda de la vida, va errando por caminos sin saber adónde.
7 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.
Pues bien, escuchadme, hijos, y no os apartéis de las palabras de mi boca;
8 Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
desvía de ella tu camino, y no te acerques a la puerta de su casa.
9 usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,
No sacrifiques tu honor a gente extraña ni tus años a un tirano,
10 wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.
no sea que extraños se harten de tus bienes, y tus fatigas beneficien a casas ajenas,
11 Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
y al fin tengas que gemir, después de consumir tu carne,
12 Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!
y hayas de exclamar: “¡Cómo he podido aborrecer la instrucción, y rehusar en mi corazón la corrección!
13 Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.
Desoí la voz de los que me adoctrinaban y no quise oír a mis maestros.
14 Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa katikati ya kusanyiko lote.”
Casi he llegado al colmo de los males, en medio del pueblo y de la asamblea.”
15 Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.
Bebe el agua de tu aljibe y los raudales que manan de tu pozo.
16 Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?
¿Por qué derramar fuera tus fuentes, por las plazas las corrientes de tu agua?
17 Na viwe vyako mwenyewe, kamwe visishirikishwe wageni.
¡Sean para ti solo, y no para los extraños a tu lado!
18 Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
¡Sea tu fuente bendita, y alégrate con la esposa de tu mocedad!
19 Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.
¡Sea ella la gacela de tu amor, una cierva graciosa, embriáguenle sus pechos perpetuamente, y su amor te encante en todo tiempo!
20 Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?
¿Por qué, hijo mío, dejarte embaucar por la mujer extraña y abrazar el seno de la ajena?
21 Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.
Pues ante Yahvé están los caminos del hombre. Él mira todos sus pasos.
22 Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.
El hombre malo será presa de sus propias iniquidades, y quedará enredado en los lazos de su pecado.
23 Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.
Perecerá por falta de disciplina, y andará perdido a causa de su gran necedad.