< Mithali 5 >
1 Mwanangu, sikiliza kwa makini hekima yangu, sikiliza vizuri maneno yangu ya busara,
我兒,你應注意我的智慧,側耳傾聽我的見解,
2 ili uweze kutunza busara na midomo yako ihifadhi maarifa.
為使你保持審慎的態度,使你的口唇能固守知識。
3 Kwa maana midomo ya mwanamke kahaba hudondoza asali, na maneno ya kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
因為淫婦的口,滴流甜蜜;她的嘴唇,比油還滑;
4 lakini mwisho wake ni mchungu kama nyongo, mkali kama upanga ukatao kuwili.
但是,與她相處的結果,卻苦若苦艾,刺心有如雙刃的利劍。
5 Miguu yake hushuka kuelekea kwenye kifo; hatua zake huelekea moja kwa moja kaburini. (Sheol )
她的雙腳陷入死境,她的腳步直趨陰府。 (Sheol )
6 Yeye hafikiri juu ya njia ya uzima; njia zake zimepotoka, lakini yeye hajui.
她不走生命的坦途;她的腳步,躊躇不定,不知所往。
7 Sasa basi wanangu, nisikilizeni; msiache ninalowaambia.
現在,我兒,你要聽從我,不要拋棄我口中的教訓:
8 Njia zenu ziwe mbali naye, msiende karibu na mlango wa nyumba yake,
你應使你的道路遠離她,不要走近她的家門,
9 usije ukatoa nguvu zako nzuri kwa wengine na miaka yako kwa aliye mkatili,
免得將你的精力,葬送給別人;將你的歲月,委棄給無賴;
10 wageni wasije wakasherehekea utajiri wako na jitihada yako ikatajirisha nyumba ya mwanaume mwingine.
免得你的財產為他人享受,你的辛勞裨益於人家;
11 Mwishoni mwa maisha yako utalia kwa uchungu, wakati nyama na mwili wako vimechakaa.
免得終期來臨,當你的肉軀和身體精力耗盡時,你只有嘆息,
12 Utasema, “Tazama jinsi gani nilivyochukia adhabu! Tazama jinsi moyo wangu ulivyodharau maonyo!
說:「唉! 為什麼我憎惡了教訓,為什麼我的心藐視了規勸﹖
13 Sikuwatii walimu wangu wala kuwasikiliza wakufunzi wangu.
為什麼我沒有聽從師長的勸告,沒有側耳傾聽教訓我的人﹖
14 Nimefika ukingoni mwa maangamizi kabisa katikati ya kusanyiko lote.”
在集會和會眾中,我幾乎陷於浩劫。」
15 Kunywa maji kutoka kwenye kisima chako mwenyewe, maji yanayotiririka kutoka kwenye kisima chako mwenyewe.
你當飲你自己池裏的水,喝你井裏的活泉。
16 Je, chemchemi zako zifurike katika barabara za mji na vijito vyako vya maji viwanjani?
你的泉水豈可外溢,成為街頭的流水﹖
17 Na viwe vyako mwenyewe, kamwe visishirikishwe wageni.
其實都應全歸於你,不得讓外人與你共享。
18 Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
你的泉源理應受祝福;你應由你少年時的妻子取樂。
19 Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.
她宛如可愛的母鹿,嫵媚的母羚;她的酥胸應常使你暢懷,她的愛情應不斷使你陶醉。
20 Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?
我兒,你為什麼要迷戀外婦,擁抱別人妻室的胸懷﹖
21 Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.
上主的眼目時常監視人的道路,不斷審察他的一切行徑。
22 Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.
惡人必被自己的邪惡所纏擾,必為自己罪惡的羅網所捕獲。
23 Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.
他必因不聽教訓而喪命,必因自己過度的愚昧而淪亡。