< Mithali 4 >
1 Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
小子等よ父の訓をきけ 聡明を知んために耳をかたむけよ
2 Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
われ善教を汝らにさづく わが律を棄つることなかれ
3 Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
われも我が父には子にして 我が母の目には獨の愛子なりき
4 baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
父われを教へていへらく我が言を汝の心にとどめ わが誡命をまもれ 然らば生べし
5 Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
智慧をえ聡明をえよ これを忘るるなかれ また我が口の言に身をそむくるなかれ
6 Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
智慧をすつることなかれ彼なんぢを守らん 彼を愛せよ彼なんぢを保たん
7 Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
智慧は第一なるものなり 智慧をえよ 凡て汝の得たる物をもて聡明をえよ
8 Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
彼を尊べ さらば彼なんぢを高く挙げん もし彼を懐かば彼汝を尊榮からしめん
9 Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
かれ美しき飾を汝の首に置き 榮の冠弁を汝に予へん
10 Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
我が子よきけ 我が言を納れよ さらば汝の生命の年おほからん
11 Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
われ智慧の道を汝に教へ義しき徑筋に汝を導けり
12 Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
歩くとき汝の歩は艱まず 趨るときも躓かじ
13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
堅く訓誨を執りて離すこと勿れ これを守れ これは汝の生命なり
14 Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
邪曲なる者の途に入ることなかれ 惡者の路をあやむこと勿れ
15 Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
これを避よ 過ること勿れ 離れて去れ
16 Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
そは彼等は惡を爲さざれば睡らず 人を躓かせざればいねず
17 Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
不義のパンを食ひ暴虐の洒を飮めばなり
18 Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
義者の途は旭光のごとし いよいよ光輝をまして昼の正午にいたる
19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
惡者の途は幽冥のごとし 彼らはその蹟くもののなになるを知ざるなり
20 Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
わが子よ我が言をきけ 我が語るところに汝の耳を傾けよ
21 Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
之を汝の目より離すこと勿れ 汝の心のうちに守れ
22 kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
是は之を得るものの生命にしてまたその全體の良薬なり
23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
すべての操守べき物よりもまさりて汝の心を守れ そは生命の流これより出ればなり
24 Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
虚偽の口を汝より棄さり 惡き口唇を汝より遠くはなせ
25 Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
汝の目は正く視 汝の眼瞼は汝の前を眞直に視るべし
26 Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
汝の足の徑をかんがへはかり 汝のすべての道を直くせよ
27 Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.
右にも左にも偏ること勿れ汝の足を惡より離れしめよ