< Mithali 4 >

1 Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
子供らよ、父の教を聞き、悟りを得るために耳を傾けよ。
2 Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
わたしは、良い教訓を、あなたがたにさずける。わたしの教を捨ててはならない。
3 Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
わたしもわが父には子であり、わが母の目には、ひとりのいとし子であった。
4 baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
父はわたしを教えて言った、「わたしの言葉を、心に留め、わたしの戒めを守って、命を得よ。
5 Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
それを忘れることなく、またわが口の言葉にそむいてはならない、知恵を得よ、悟りを得よ。
6 Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
知恵を捨てるな、それはあなたを守る。それを愛せよ、それはあなたを保つ。
7 Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
知恵の初めはこれである、知恵を得よ、あなたが何を得るにしても、悟りを得よ。
8 Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
それを尊べ、そうすれば、それはあなたを高くあげる、もしそれをいだくならば、それはあなたを尊くする。
9 Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
それはあなたの頭に麗しい飾りを置き、栄えの冠をあなたに与える」。
10 Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
わが子よ、聞け、わたしの言葉をうけいれよ、そうすれば、あなたの命の年は多くなる。
11 Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
わたしは知恵の道をあなたに教え、正しい道筋にあなたを導いた。
12 Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
あなたが歩くとき、その歩みは妨げられず、走る時にも、つまずくことはない。
13 Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
教訓をかたくとらえて、離してはならない、それを守れ、それはあなたの命である。
14 Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
よこしまな者の道に、はいってはならない、悪しき者の道を歩んではならない。
15 Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
それを避けよ、通ってはならない、それを離れて進め。
16 Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
彼らは悪を行わなければ眠ることができず、人をつまずかせなければ、寝ることができず、
17 Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
不正のパンを食らい、暴虐の酒を飲むからである。
18 Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
正しい者の道は、夜明けの光のようだ、いよいよ輝きを増して真昼となる。
19 Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
悪しき人の道は暗やみのようだ、彼らは何につまずくかを知らない。
20 Mwanangu, yasikilize kwa makini yale ninayokuambia; sikiliza kwa makini maneno yangu.
わが子よ、わたしの言葉に心をとめ、わたしの語ることに耳を傾けよ。
21 Usiruhusu yaondoke machoni pako, yahifadhi ndani ya moyo wako;
それを、あなたの目から離さず、あなたの心のうちに守れ。
22 kwa sababu ni uzima kwa wale wanaoyapata na afya kwa mwili wote wa mwanadamu.
それは、これを得る者の命であり、またその全身を健やかにするからである。
23 Zaidi ya yote, linda moyo wako, kuliko yote uyalindayo, maana ndiko zitokako chemchemi za uzima.
油断することなく、あなたの心を守れ、命の泉は、これから流れ出るからである。
24 Epusha kinywa chako na ukaidi; weka mazungumzo machafu mbali na midomo yako.
曲った言葉をあなたから捨てさり、よこしまな談話をあなたから遠ざけよ。
25 Macho yako na yatazame mbele, kaza macho yako moja kwa moja mbele yako.
あなたの目は、まっすぐに正面を見、あなたのまぶたはあなたの前を、まっすぐに見よ。
26 Sawazisha mapito ya miguu yako na njia zako zote ziwe zimethibitika.
あなたの足の道に気をつけよ、そうすれば、あなたのすべての道は安全である。
27 Usigeuke kulia wala kushoto; epusha mguu wako na ubaya.
右にも左にも迷い出てはならない、あなたの足を悪から離れさせよ。

< Mithali 4 >