< Mithali 31 >
1 Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
Ķēniņa Lemuēļa vārdi, tā mācība, ko viņa māte tam mācīja.
2 “Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
Ak, mans dēls! ak manas miesas dēls! tu manu solījumu dēls.
3 Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
Nedod sievām savu spēku, nedz savu ceļu tām, kas ķēniņus samaitā.
4 “Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
Ķēniņiem nebūs, ak Lemuēl, ķēniņiem nebūs vīna dzert, nedz valdniekiem stipra dzēriena iekārot,
5 wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
Ka dzerdami neaizmirst likumus, un nepārgroza tiesu visiem sērdieņiem.
6 Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
Dodiet stipru dzērienu tam, kas iet bojā, un vīnu, kam noskumusi sirds:
7 Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
Tāds lai dzer, ka aizmirst savu nabadzību, un vairs nepiemin savas bēdas.
8 “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
Atdari savu muti par mēmo un par visiem, kas ir atstāti.
9 Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
Atdari savu muti, tiesā taisni un nes tiesu nabagam un sērdienim.
10 Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
Tikušu (tikumīgu) sievu, kas tādu atrod, pāri par pērlēm ir viņas dārgums.
11 Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
Uz viņu uzticas vīra sirds un labuma tam netrūkst nekāda.
12 Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
Tā dara tam labu, ne ļaunu visās sava mūža dienās.
13 Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
Viņa gādā par vilnu un liniem un strādā priecīgām rokām.
14 Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
Tā ir kā laivinieka laiva, sagādā maizi no tālienes.
15 Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
Jau pašā naktī tā ceļas un dod barību savai saimei un kalponēm iespriesto tiesu.
16 Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
To zemes stūri, ko cerē, tā dabū, no savu roku augļiem tā dēsta vīna dārzu.
17 Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
Ar spēku tā jož savus gurnus un savas rokas ar stiprumu.
18 Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
Tā mana, ka viņas pūliņš labi sokas, un gaisma tai neapdziest naktī.
19 Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
Tā stiepj savu roku pie kodeļa un tver ar pirkstiem ratiņu.
20 Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
Tā sērdieņus mīlīgi apkampj un pasniedz nabagiem roku.
21 Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
Savam namam tā nebīstas sniega, jo saime divkārtīgi ģērbta.
22 Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
Tā sev taisa apsegus, dārgs audeklis un purpurs tai ir apģērbs.
23 Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
Tai vīrs ir pazīstams vārtos, kad tas sēž ar zemes vecajiem.
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
Viņa auž linu svārkus un pārdod, un izdod pircējiem jostas.
25 Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
Stiprums un gods tai apģērbs; tā smejas par nākamo laiku.
26 Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
Savu muti tā atdara ar gudrību, un uz viņas mēles ir jauka mācība.
27 Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
Viņa skatās pēc visām sava nama gaitām un neēd savu maizi ar slinkumu.
28 Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
Viņas bērni pieceļas un teic viņu laimīgu; viņas vīrs, tas to slavē:
29 “Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
Daudz mātes meitām ir goda tikums, bet tu esi pāri par visām!
30 Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
Daiļums viļ un skaistums paiet; dievbijīga sieva, tā ir teicama!
31 Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.
Teiciet viņu par viņas roku augļiem, un viņas pašas darbi lai viņu ļaudīs teic!