< Mithali 31 >
1 Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
Siangpahrang Lemuel lawk, a manu ni a cangkhai e naw teh:
2 “Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
Bangtelane ka capa, bangtelane ka khe e capa, bangtelane ka lawkkam capa.
3 Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
Siangpahrangnaw patenghai karaphoekung napui koe na thaonae poe hanh.
4 “Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
Aw Lemuel, misurtui nei e hoi yamu nei e teh siangpahrangnaw hane nahoeh.
5 wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
Hoehpawiteh, net awh vaiteh kâlawk pahnim awh vaiteh mathoenaw hanelah kalanhoehe lah lawkceng awh langvaih.
6 Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
Meimei kadout e hah yamu pânei awh nateh, lungrei ka thai e hah misurtui pânei awh.
7 Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
Net awh naseh, a reithainae hah pahnim awh naseh, a lungmathoenae pahnim totouh net awh naseh.
8 “Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
Lawkanaw hanlah dei pouh nateh, due hanelah lawk tâtueng pouh e naw hane hai dei pouh.
9 Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
Kalan lah lawkceng nateh tamimathoe hoi tamikavout hanlah kâhet pouh.
10 Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
Yu kahawi apinimaw a hmu thai han. Bangkongtetpawiteh talung phukaawm hlak hai aphuohnawn.
11 Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
A vâ ni a lungthin hoi a kâuep teh hawinae awm laipalah awm mahoeh.
12 Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
A hring nathung thoenae laipalah hawinae dueng doeh a sak pouh.
13 Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
Tumuen hoi pahla hah a tawng teh a kut hoi amahmawk ouk a tawk.
14 Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
Hno ka yawt e long patetlah ao teh, ahlanae koehoi rawca ouk a thokhai.
15 Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
Amom a thaw teh a imthungnaw hah rawca a paca teh, a sannunaw hah thaw rip a boun.
16 Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
Lawhmuen hah a khet teh a ran, a tawkphu hoi misur takha a sak.
17 Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
A keng dawk tha a kâyeng teh, a kuttha hai a patung.
18 Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
Hno a yo e a mek tie a panue dawkvah tangmin patenghai hmaiim dout hoeh.
19 Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
A kut hoi rahakut a kuet teh, avanglae kut hoi yâcung a kuet.
20 Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
Tamimathoe hanelah a kut a kâyap, bokheiyah kavoutnaw totouh a kut ni koung a pha.
21 Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
Tadamtui ka bawt nakunghai a imthungnaw hanelah taki hane awm hoeh, bangkongtetpawiteh a imthungnaw ni dikpalingca e khohna kabet e a khohna awh.
22 Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
Ama hanlah hni a kawng teh, loukloukkaang e hoi pu doeh a khohna.
23 Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
A vâ hai kho longkha koe khobawinaw hoi a tahung toteh mithmaiben e lah ao.
24 Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
Loukloukkaang e hni a kawng teh a yo, hno kayawtnaw koe taisawm hah a yo.
25 Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
A kawng e khohna teh a khaw, ahawi dawkvah ahni teh hmalah a konawm han.
26 Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
Lungangnae hoi lawk a dei, a lawk teh pahrennae kâlawk lah ao.
27 Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
A imthung khosaknae kahawicalah koung a khetyawt, rawca hai pamda laihoi cat boihoeh.
28 Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
A canaw a thaw awh teh a manu koe a lunghawi awh. A vâ ni hai a oup van,
29 “Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
napui kapap ni kahawicalah a tawk awh toe, hatei nang ni ahnimanaw na tapuet toe, atipouh.
30 Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
Raimonae teh dumnae doeh, meihawinae hai a yawmyin doeh. Hatei BAWIPA ka taket e napui teh oup lah ao han.
31 Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.
A kut hoi a tawk e a paw hah poe awh nateh, longkha koe ama roeroe hah a tawk e ni oup naseh.