< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Mon fils, n’oublie pas ma loi, et que ton cœur garde mes préceptes,
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Car ils t’apporteront la longueur des jours, des années de vie, et la paix.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Que la miséricorde et la vérité ne t’abandonnent pas: mets-les autour de ton cou, grave-les sur les tables de ton cœur:
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Et tu trouveras grâce et une bonne discipline devant Dieu et les hommes.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Aie confiance dans le Seigneur de tout ton cœur, et ne t’appuie pas sur ta prudence.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
Dans toutes tes voies, pense à lui, et lui-même dirigera tes pas.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Ne sois pas sage à tes propres yeux: crains Dieu, et éloigne-toi du mal;
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
Car ce sera la santé pour ton corps et une irrigation pour tes os.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Honore le Seigneur de ton bien, et donne-lui des prémices de tous tes fruits;
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
Et tes greniers seront remplis d’abondance, et tes pressoirs regorgeront de vin.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
Ne rejetteras, mon fils, la discipline du Seigneur: et ne te décourage pas, lorsque par lui tu es châtié;
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
Car le Seigneur châtie celui qu’il aime, et il se complaît en lui comme un père en son fils.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Bienheureux l’homme qui a trouvé la sagesse, et qui est riche en prudence:
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
L’acquisition de la sagesse vaut mieux que le commerce de l’argent, et ses fruits sont préférables à l’or le meilleur et le plus pur;
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
Elle est plus précieuse que toutes les richesses; et tout ce qu’on désire ne peut lui être comparé.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
La longueur des jours est dans sa droite; et dans sa gauche sont les richesses et la gloire.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Ses voies sont des voies belles, et tous ses sentiers sont pacifiques.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
Elle est un arbre de vie pour ceux qui la saisissent, et celui qui la tient est bienheureux.
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
Le Seigneur, par la sagesse, a fondé la terre: il a affermi les cieux par la prudence.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
Par sa sagesse ont paru tout à coup des abîmes, et les nuées se chargent de rosée.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
Mon fils, que ces choses ne s’éloignent pas de tes yeux; garde la loi et le conseil;
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
Et ce sera la vie pour ton âme, et un ornement à ton cou;
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Alors tu marcheras avec assurance dans ta voie, et ton pied ne se heurtera pas;
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
Si tu dors, tu ne craindras pas: tu reposeras, et doux sera ton sommeil;
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
Ne redoute pas une terreur soudaine, ni les puissances des impies fondant sur toi.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
Car le Seigneur sera à ton côté, et il gardera ton pied, afin que tu ne sois point pris.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
N’empêche point de bien faire celui qui le peut: si tu es en état, fais toi-même bien.
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
Ne dis pas à ton ami: Va et reviens; demain je te donnerai, lorsqu’à l’instant tu peux donner.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Ne machine pas de mal contre ton ami, puisque lui en toi a confiance.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
Ne dispute pas avec un homme sans sujet, lorsque lui-même ne t’a rien fait de mal.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Ne porte pas envie à un homme injuste, et n’imite pas ses voies,
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
Parce que c’est l’abomination du Seigneur, qu’un moqueur; et que c’est avec les simples qu’est sa conversation.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
La détresse viendra du Seigneur dans la maison de l’impie; mais les habitations des justes seront bénies.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Il se jouera lui-même des moqueurs; et aux hommes doux il donnera sa grâce.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Les sages posséderont la gloire: l’élévation des insensés sera l’ignominie.

< Mithali 3 >