< Mithali 3 >
1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
O son my instruction my may not you forget and commandments my let it keep heart your.
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
For length of days and years of life and peace they will add to you.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Loyalty and faithfulness may not they leave you bind them on necks your write them on [the] tablet of heart your.
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
And find favor and insight good in [the] eyes of God and humankind.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Trust to Yahweh with all heart your and to own understanding your may not you depend.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
In all ways your acknowledge him and he he will make straight paths your.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
May not you be wise in own eyes your fear Yahweh and turn aside from evil.
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
Healing may it be to navel your and refreshment to bones your.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Honor Yahweh from wealth your and from [the] first of all produce your.
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
So they may be filled storehouses your plenty and new wine wine vats your they will burst open.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
[the] discipline of Yahweh O son my may not you reject and may not you loath rebuke his.
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
For [the one] whom he loves Yahweh he reproves and like a father a son [whom] he is pleased with.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
How blessed! [is] a person [who] he finds wisdom and a person [who] he obtains understanding.
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
For [is] good profit her more than [the] profit of silver and more than gold gain her.
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
[is] precious She (more than jewels *Q(k)*) and all pleasures your not they compare with her.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Length of days [is] in right [hand] her [are] in left [hand] her wealth and honor.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Ways her [are] ways of kindness and all pathways her [are] well-being.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
[is] a tree of Life she to [those who] take hold on her and [those who] hold fast to her [are] called blessed.
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
Yahweh by wisdom he founded [the] earth he established [the] heavens by understanding.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
By knowledge his [the] depths they were split open and clouds they dripped dew.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
O son my may not they depart from eyes your keep sound wisdom and discretion.
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
So they may be life for self your and grace for neck your.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Then you will walk to security way your and foot your not it will strike.
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
If you will lie down not you will fear and you will lie down and it will be pleasing sleep your.
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
May not you be afraid from terror suddenly and from [the] devastation of wicked [people] that it will come.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
For Yahweh he will be confidence your and he will keep foot your from capture.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
May not you withhold good from owners its when belongs to [the] power of (hand your *Q(K)*) to do [it].
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
May not you say (to neighbor your *Q(K)*) go and come back and tomorrow I will give [it] and there is with you.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
May not you devise on neighbor your harm and he [is] dwelling to security with you.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
May not (you contend *Q(k)*) with anyone without cause if not he has dealt out to you evil.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
May not you be jealous of a person of violence and may not you choose all ways his.
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
For [is] [the] abomination of Yahweh a crooked [person] and [is] with upright [people] intimacy his.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
[the] curse of Yahweh [is] on [the] house of [the] wicked and [the] habitation of righteous [people] he blesses.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Though mockers he he mocks (and to humble [people] *Q(K)*) he gives favor.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
Honor wise [people] they will inherit and fools [is] lifting up shame.