< Mithali 3 >
1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
My sonne, forget not thou my Lawe, but let thine heart keepe my commandements.
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
For they shall increase the length of thy dayes and the yeeres of life, and thy prosperitie.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Let not mercie and trueth forsake thee: binde them on thy necke, and write them vpon the table of thine heart.
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
So shalt thou finde fauour and good vnderstanding in the sight of God and man.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Trust in the Lord with all thine heart, and leane not vnto thine owne wisdome.
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
In all thy wayes acknowledge him, and he shall direct thy wayes.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Be not wise in thine owne eyes: but feare the Lord, and depart from euill.
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
So health shalbe vnto thy nauel, and marowe vnto thy bones.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Honour the Lord with thy riches, and with the first fruites of all thine increase.
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
So shall thy barnes be filled with abundance, and thy presses shall burst with newe wine.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
My sonne, refuse not the chastening of the Lord, neither be grieued with his correction.
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
For the Lord correcteth him, whome he loueth, euen as the father doeth the childe in whom he deliteth.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Blessed is the man that findeth wisedome, and the man that getteth vnderstanding.
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
For the marchandise thereof is better then the marchandise of siluer, and the gaine thereof is better then golde.
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
It is more precious then pearles: and all things that thou canst desire, are not to be compared vnto her.
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
Length of dayes is in her right hand, and in her left hand riches and glory.
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
Her wayes are wayes of pleasure, and all her pathes prosperitie.
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
She is a tree of life to them that lay holde on her, and blessed is he that retaineth her.
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
The Lord by wisdome hath layde the foundation of the earth, and hath stablished the heauens through vnderstanding.
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
By his knowledge the depthes are broken vp, and the cloudes droppe downe the dewe.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
My sonne, let not these things depart from thine eyes, but obserue wisdome, and counsell.
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
So they shalbe life to thy soule, and grace vnto thy necke.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Then shalt thou walke safely by thy way: and thy foote shall not stumble.
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
If thou sleepest, thou shalt not bee afraide, and when thou sleepest, thy sleepe shalbe sweete.
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
Thou shalt not feare for any sudden feare, neither for the destruction of the wicked, when it commeth.
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
For the Lord shall be for thine assurance, and shall preserue thy foote from taking.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
Withhold not the good from the owners thereof, though there be power in thine hand to doe it.
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
Say not vnto thy neighbour, Go and come againe, and to morow wil I giue thee, if thou now haue it.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Intend none hurt against thy neighbour, seeing he doeth dwell without feare by thee.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
Striue not with a man causelesse, when he hath done thee no harme.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Bee not enuious for the wicked man, neither chuse any of his wayes.
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
For the frowarde is abomination vnto the Lord: but his secret is with the righteous.
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
The curse of the Lord is in the house of the wicked: but he blesseth the habitation of the righteous.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
With the scornefull he scorneth, but hee giueth grace vnto the humble.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
The wise shall inherite glorie: but fooles dishonour, though they be exalted.