< Mithali 3 >

1 Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
Min Søn, glem ikke, hvad jeg har lært dig, dit Hjerte tage vare paa mine Bud!
2 kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
Thi en Række af Dage og Leveaar og Lykke bringer de dig.
3 Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
Godhed og Troskab vige ej fra dig, bind dem som Baand om din Hals, skriv dem paa dit Hjertes Tavle!
4 Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
Saa finder du Naade og Yndest i Guds og Menneskers Øjne.
5 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
Stol paa HERREN af hele dit Hjerte, men forlad dig ikke paa din Forstand;
6 katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
hav ham i Tanke paa alle dine Veje, saa jævner han dine Stier.
7 Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
Hold ikke dig selv for viis, frygt HERREN og vig fra det onde;
8 Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
saa faar du Helse for Legemet, Lindring for dine Ledemod.
9 Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
Ær med din Velstand HERREN med Førstegrøden af al din Avl;
10 ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
da fyldes dine Lader med Korn, dine Perser svømmer over af Most.
11 Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
Min Søn, lad ej haant om HERRENS Tugt, vær ikke ked af hans Revselse;
12 kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
HERREN revser den, han elsker, han straffer den Søn, han har kær.
13 Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
Lykkelig den, der har opnaaet Visdom, den, der vinder sig Indsigt;
14 kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
thi den er bedre at købe end Sølv, bedre at vinde end Guld;
15 Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
den er mere værd end Perler, ingen Klenodier opvejer den;
16 Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
en Række af Dage er i dens højre, i dens venstre Rigdom og Ære;
17 Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
dens Veje er liflige Veje, og alle dens Stier er Lykke;
18 Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
den er et Livets Træ for dem, der griber den, lykkelig den, som holder den fast!
19 Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
HERREN grundlagde Jorden med Visdom, grundfæsted Himlen med Indsigt;
20 kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
ved hans Kundskab brød Strømmene frem, lader Skyerne Dug dryppe ned.
21 Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
Min Søn, tag Vare paa Snilde og Kløgt, de slippe dig ikke af Syne;
22 ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
saa bliver de Liv for din Sjæl og et yndigt Smykke til din Hals.
23 Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
Da vandrer du trygt din Vej, støder ikke imod med din Fod;
24 ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
sætter du dig, skal du ikke skræmmes, lægger du dig, skal din Søvn vorde sød;
25 Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
du skal ikke frygte uventet Rædsel, Uvejret, naar det kommer over gudløse;
26 kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
thi HERREN skal være din Tillid, han vogter din Fod, saa den ikke hildes.
27 Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
Nægt ikke den trængende Hjælp, naar det staar i din Magt at hjælpe;
28 Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
sig ej til din Næste: »Gaa og kom igen, jeg vil give i Morgen!« — saafremt du har det.
29 Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
Tænk ikke paa ondt mod din Næste, naar han tillidsfuldt bor i din Nærhed.
30 Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
Yp ikke Trætte med sagesløs Mand, naar han ikke har voldet dig Men.
31 Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
Misund ikke en Voldsmand, græm dig aldrig over hans Veje;
32 kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
thi den falske er HERREN en Gru; mod retsindig er han fortrolig;
33 Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
i den gudløses Hus er HERRENS Forbandelse, men retfærdiges Bolig velsigner han.
34 Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
Over for Spottere bruger han Spot, men ydmyge giver han Naade.
35 Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.
De vise faar Ære til Arv, men Taaber høster kun Skam.

< Mithali 3 >