< Mithali 29 >
1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
EL hombre que reprendido endurece la cerviz, de repente será quebrantado; ni habrá [para él] medicina.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Cuando los justos dominan, el pueblo se alegra: mas cuando domina el impío, el pueblo gime.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
El hombre que ama la sabiduría, alegra á su padre: mas el que mantiene rameras, perderá la hacienda.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
El rey con el juicio afirma la tierra: mas el hombre de presentes la destruirá.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
El hombre que lisonjea á su prójimo, red tiende delante de sus pasos.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
En la prevaricación del hombre malo hay lazo: mas el justo cantará y se alegrará.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Conoce el justo la causa de los pobres: [mas] el impío no entiende sabiduría.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Los hombres escarnecedores enlazan la ciudad: mas los sabios apartan la ira.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Si el hombre sabio contendiere con el necio, que se enoje ó que se ría, no tendrá reposo.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Los hombres sanguinarios aborrecen al perfecto: mas los rectos buscan su contentamiento.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
El necio da suelta á todo su espíritu; mas el sabio al fin le sosiega.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Del señor que escucha la palabra mentirosa, todos sus ministros son impíos.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
El pobre y el usurero se encontraron: Jehová alumbra los ojos de ambos.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
El rey que juzga con verdad á los pobres, su trono será firme para siempre.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La vara y la corrección dan sabiduría: mas el muchacho consentido avergonzará á su madre.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Cuando los impíos son muchos, mucha es la prevaricación; mas los justos verán la ruina de ellos.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Corrige á tu hijo, y te dará descanso, y dará deleite á tu alma.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Sin profecía el pueblo será disipado: mas el que guarda la ley, bienaventurado él.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
El siervo no se corregirá con palabras: porque entiende, mas no corresponde.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
¿Has visto hombre ligero en sus palabras? más esperanza hay del necio que de él.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
El que regala á su siervo desde su niñez, á la postre será su hijo.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
El hombre iracundo levanta contiendas; y el furioso muchas veces peca.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
La soberbia del hombre le abate; pero al humilde de espíritu sustenta la honra.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
El aparcero del ladrón aborrece su vida; oirá maldiciones, y no [lo] denunciará.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
El temor del hombre pondrá lazo: mas el que confía en Jehová será levantado.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Muchos buscan el favor del príncipe: mas de Jehová [viene] el juicio de cada uno.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Abominación es á los justos el hombre inicuo; y abominación es al impío el de rectos caminos.