< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
Vīrs, kas pārmācīts, tomēr ciets, taps piepeši salauzts, un nebūs, kas dziedina.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Kad taisnie iet vairumā, tad ļaudis priecājās; bet kad bezdievīgais valda, tad ļaudis nopūšās.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
Kas gudrību mīļo, iepriecina savu tēvu; bet kas ar maukām pinās, tas izplītē savu mantu.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Caur tiesu un taisnību ķēniņš dara valsti pastāvam; bet kas dāvanas plēš, tas to izposta.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
Kas otram mīksti pieglaužas, met tīklu viņa soļiem.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Bezdievīgais savaldzinājās savos grēkos, bet taisnais priecājās un līksmojās.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Taisnais ņem vērā nabaga žēlošanos; bezdievīgais par to nemaz nebēdā.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Kam viss tik smiekls, sakurina pilsētu; bet gudrie apslāpē kaislību.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Gudrs ar ģeķi pie tiesas, tad skaistās, tad smejas, galā netiek.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Asins vīri ienīst bezvainīgo, bet taisnie rūpējās par viņa dvēseli.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
Ģeķis izkrata visu savu padomu, bet gudrs vīrs to patur pie sevis.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Kungs, kas uz meliem klausa, tam visi kalpi blēži.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Nabagi un mantas plēsēji sastop viens otru; abiem Tas Kungs dod acu gaismu.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Ķēniņš, kas nabagiem nes taisnu tiesu, tā goda krēsls pastāvēs mūžīgi.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
Rīkste un pārmācība dod gudrību; bet bērns savā vaļā dara mātei kaunu.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Kur bezdievīgie iet vairumā, tur vairojās grēki; bet taisnie redzēs viņu krišanu.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Pārmāci savu dēlu, tad tev būs prieks no viņa un tavai dvēselei līksmība.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Kur Dieva mācības nav, tur ļaudis nevaldāmi; bet svētīgs, kas mācību sargā.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Kalps ar vārdiem nav mācams; lai gan labi prot, taču neklausa,
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Kad tu vīru redzi, kam veikla mēle, tad no muļķa vairāk cerības nekā no tāda.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Kad kalpu no pirmā gala izlutina, tad pēcgalā grib būt par pašu dēlu.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
Ātrs cilvēks saceļ bāršanos, un sirdīgs vīrs padara daudz grēku.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
Cilvēka lepnība viņu gāzīs, bet pazemīgs gars panāks godu.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Kas ar zagli dalās, tas ienīst savu dvēseli; viņš dzird Dieva lāstus un nepierāda.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
Priekš cilvēkiem drebēt ieved valgos; bet kas uz To Kungu paļaujas, ir drošā vietā.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Daudzi meklē valdnieka vaigu; bet no Tā Kunga nāk katram tā tiesa.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Netaisnais riebj taisniem, un kas bezvainīgs savā ceļā, riebj bezdievīgam.

< Mithali 29 >