< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
viro qui corripientem dura cervice contemnit repentinus superveniet interitus et eum sanitas non sequitur
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
in multiplicatione iustorum laetabitur vulgus cum impii sumpserint principatum gemet populus
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
vir qui amat sapientiam laetificat patrem suum qui autem nutrit scorta perdet substantiam
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
rex iustus erigit terram vir avarus destruet eam
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
homo qui blandis fictisque sermonibus loquitur amico suo rete expandit gressibus eius
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
peccantem virum iniquum involvet laqueus et iustus laudabit atque gaudebit
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
novit iustus causam pauperum impius ignorat scientiam
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
homines pestilentes dissipant civitatem sapientes avertunt furorem
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
vir sapiens si cum stulto contenderit sive irascatur sive rideat non inveniet requiem
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
viri sanguinum oderunt simplicem iusti quaerunt animam eius
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
totum spiritum suum profert stultus sapiens differt et reservat in posterum
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
princeps qui libenter audit verba mendacii omnes ministros habebit impios
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
pauper et creditor obviam fuerunt sibi utriusque inluminator est Dominus
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
rex qui iudicat in veritate pauperes thronus eius in aeternum firmabitur
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
virga atque correptio tribuet sapientiam puer autem qui dimittitur voluntati suae confundet matrem suam
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
in multiplicatione impiorum multiplicabuntur scelera et iusti ruinas eorum videbunt
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
erudi filium tuum et refrigerabit te et dabit delicias animae tuae
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
cum prophetia defecerit dissipabitur populus qui custodit legem beatus est
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
servus verbis non potest erudiri quia quod dicis intellegit et respondere contemnit
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
vidisti hominem velocem ad loquendum stulti magis speranda est quam illius correptio
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
qui delicate a pueritia nutrit servum suum postea illum sentiet contumacem
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
vir iracundus provocat rixas et qui ad indignandum facilis est erit ad peccata proclivior
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
superbum sequitur humilitas et humilem spiritu suscipiet gloria
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
qui cum fure partitur odit animam suam adiurantem audit et non indicat
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
qui timet hominem cito corruet qui sperat in Domino sublevabitur
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
multi requirunt faciem principis et a Domino iudicium egreditur singulorum
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
abominantur iusti virum impium et abominantur impii eos qui in recta sunt via

< Mithali 29 >