< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
Viro, qui corripientem dura cervice contemnit, repentinus ei superveniet interitus: et eum sanitas non sequetur.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
In multiplicatione iustorum lætabitur vulgus: cum impii sumpserint principatum, gemet populus.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
Vir, qui amat sapientiam, lætificat patrem suum: qui autem nutrit scorta, perdet substantiam.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Rex iustus erigit terram, vir avarus destruet eam.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
Homo, qui blandis, fictisque sermonibus loquitur amico suo, rete expandit gressibus eius.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Peccantem virum iniquum involvet laqueus: et iustus laudabit atque gaudebit.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Novit iustus causam pauperum: impius ignorat scientiam.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Homines pestilentes dissipant civitatem: sapientes vero avertunt furorem.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Vir sapiens, si cum stulto contenderit, sive irascatur, sive rideat, non inveniet requiem.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Viri sanguinum oderunt simplicem: iusti autem quærunt animam eius.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
Totum spiritum suum profert stultus: sapiens differt, et reservat in posterum.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Princeps, qui libenter audit verba mendacii, omnes ministros habet impios.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Pauper, et creditor obviaverunt sibi: utriusque illuminator est Dominus.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Rex, qui iudicat in veritate pauperes, thronus eius in æternum firmabitur.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
Virga atque correptio tribuit sapientiam: puer autem, qui dimittitur voluntati suæ, confundit matrem suam.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
In multiplicatione impiorum multiplicabuntur scelera: et iusti ruinas eorum videbunt.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Erudi filium tuum, et refrigerabit te, et dabit delicias animæ tuæ.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Cum prophetia defecerit, dissipabitur populus: qui vero custodit legem, beatus est.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Servus verbis non potest erudiri: quia quod dicis intelligit, et respondere contemnit.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Vidisti hominem velocem ad loquendum? stultitia magis speranda est, quam illius correptio.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Qui delicate a pueritia nutrit servum suum, postea sentiet eum contumacem.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
Vir iracundus provocat rixas: et qui ad indignandum facilis est, erit ad peccandum proclivior.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
Superbum sequitur humilitas: et humilem spiritu suscipiet gloria.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Qui cum fure participat, odit animam suam: adiurantem audit, et non indicat.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
Qui timet hominem, cito corruet: qui sperat in Domino, sublevabitur.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Multi requirunt faciem principis: et iudicium a Domino egreditur singulorum.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Abominantur iusti virum impium: et abominantur impii eos, qui in recta sunt via. Verbum custodiens filius, extra perditionem erit.

< Mithali 29 >