< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
À l’homme qui avec un cou roide méprise celui qui le reprend, surviendra une mort soudaine; et la guérison ne le suivra pas.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
À la multiplication des justes tout le monde se réjouira; lorsque les impies prendront le gouvernement, le peuple gémira.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
L’homme qui aime la sagesse réjouit son père; mais celui qui nourrit des prostituées perdra son bien.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Un roi juste élève un pays; un homme avare le détruira.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
L’homme qui parle à son ami en des termes flatteurs et déguisés tend un filet à ses pieds.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
L’homme inique qui pèche, un lacs l’enveloppera; et le juste louera le Seigneur et se réjouira.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Le juste connaît la cause des pauvres; l’impie ignore la science.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Les hommes pernicieux détruisent une cité; mais les sages détournent la fureur.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Un homme sage, s’il dispute avec un insensé, soit qu’il s’irrite, soit qu’il rie, ne trouvera pas de repos.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Les hommes de sang haïssent le simple; mais les justes cherchent son âme.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
L’insensé met tout de suite en avant son esprit; mais le sage diffère et réserve pour l’avenir.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Le prince qui écoute volontiers des paroles de mensonge a tous ses ministres impies.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Le pauvre et le créancier se sont rencontrés; celui qui éclaire l’un et l’autre, c’est le Seigneur.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Le roi qui juge selon la vérité les pauvres, son trône sera à jamais affermi.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La verge et la correction donnent la sagesse; mais l’enfant, abandonné à sa volonté, couvre de confusion sa mère.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Par la multiplication des impies se multiplieront les crimes; et les justes verront leur ruine.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Forme ton fils, et il te consolera, et il fera les délices de ton âme.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Lorsque la prophétie cessera, le peuple sera dissipé; mais celui qui garde la loi est bienheureux.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
L’esclave, par des paroles, ne peut être formé; parce qu’il comprend ce que tu dis, et il dédaigne de répondre.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
As-tu vu un homme prompt à parler? Il faut en attendre de la folie plutôt que son amendement.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Celui qui, dès l’enfance, nourrit délicatement son esclave le trouvera dans la suite rebelle.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
L’homme colère provoque des rixes; et celui qui est facile à s’indigner sera plus enclin à pécher.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
L’humiliation suit le superbe; et la gloire accueillera l’humble d’esprit.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Celui qui avec un voleur s’associe hait sa propre âme; il entend celui qui l’adjure, et il ne décèle pas le voleur.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
Celui qui craint l’homme tombera promptement; celui qui espère dans le Seigneur sera élevé.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Beaucoup recherchent la face du prince; mais c’est du Seigneur que procède le jugement de chacun.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Les justes abominent l’homme impie; et les impies abominent ceux qui sont dans la droite voie. Le fils qui garde la parole sera hors de perdition.

< Mithali 29 >