< Mithali 29 >
1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
L'homme qui, étant repris, roidit son cou, sera subitement brisé, sans qu'il y ait de guérison.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Quand les justes sont les plus nombreux, le peuple se réjouit; mais quand le méchant domine, le peuple gémit.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
L'homme qui aime la sagesse, réjouit son père; mais celui qui se plaît avec les débauchées, dissipe ses richesses.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Le roi affermit le pays par la justice; mais celui qui aime les présents le ruine.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
L'homme qui flatte son prochain, tend un filet sous ses pas.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Il y a un piège dans le crime du méchant; mais le juste chante et se réjouit.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Le juste prend connaissance de la cause des pauvres; mais le méchant ne s'en informe pas.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Les hommes moqueurs soufflent le feu dans la ville; mais les sages calment la colère.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Un homme sage contestant avec un homme insensé, qu'il se fâche ou qu'il rie, n'aura point de repos.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Les hommes sanguinaires haïssent l'homme intègre; mais les hommes droits protègent sa vie.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
L'insensé met dehors tout ce qu'il a dans l'esprit; mais le sage le réprime et le retient.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Quand le prince prête l'oreille à la parole de mensonge, tous ses serviteurs sont méchants.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Le pauvre et l'oppresseur se rencontrent; c'est l'Éternel qui éclaire les yeux de l'un et de l'autre.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Le trône du roi qui rend justice aux pauvres selon la vérité, sera affermi à perpétuité.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La verge et la répréhension donnent la sagesse; mais l'enfant livré à lui-même fait honte à sa mère.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Quand les méchants sont les plus nombreux, les crimes se multiplient; mais les justes verront leur ruine.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Corrige ton enfant, et il te donnera du repos, et il fera la joie de ton âme.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Lorsqu'il n'y a point de vision, le peuple est sans frein; mais heureux est celui qui garde la loi!
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Ce n'est pas par des paroles qu'on corrige un esclave; car il entend bien, mais ne répond pas.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
As-tu vu un homme étourdi dans ses paroles? Il y a plus à espérer d'un fou que de lui.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Le serviteur sera à la fin le fils de celui qui le nourrit délicatement dès la jeunesse.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
L'homme colère excite les querelles, et l'homme emporté commet bien des fautes.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
L'orgueil de l'homme l'abaisse; mais celui qui est humble d'esprit, obtient la gloire.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Celui qui partage avec un larron, hait son âme; il entend le serment d'exécration, et il ne déclare rien.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
La crainte qu'on a de l'homme, fait tomber dans le piège; mais celui qui s'assure en l'Éternel aura une haute retraite.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Plusieurs recherchent la faveur de celui qui domine; mais c'est l'Éternel qui fait droit à chacun.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
L'homme inique est en abomination aux justes, et celui qui va droit est en abomination au méchant.