< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
L’homme qui, étant souvent repris, roidit son cou, sera brisé subitement, et il n’y a pas de remède.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Quand les justes se multiplient, le peuple se réjouit; mais quand le méchant gouverne, le peuple gémit.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
L’homme qui aime la sagesse est la joie de son père, mais le compagnon des prostituées dissipera son bien.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Un roi, par le juste jugement, affermit le pays, mais l’homme qui accepte des présents le ruine.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
L’homme qui flatte son prochain étend un filet devant ses pas.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Dans la transgression de l’homme mauvais, il y a un piège; mais le juste chantera et se réjouira.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Le juste prend connaissance de la cause des pauvres; le méchant ne comprend aucune connaissance.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Les hommes moqueurs mettent en feu une ville, mais les sages détournent la colère.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Un homme sage qui plaide avec un homme insensé, qu’il s’irrite ou qu’il rie, n’a point de repos.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Les hommes de sang haïssent l’homme intègre, mais les hommes droits tiennent à sa vie.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
Le sot met dehors tout son esprit, mais le sage le calme et le retient.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Qu’un gouverneur prête attention à la parole de mensonge, tous ses serviteurs seront méchants.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Le pauvre et l’oppresseur se rencontrent, l’Éternel éclaire les yeux de tous deux.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Le roi qui juge les pauvres selon la vérité, … son trône sera affermi pour toujours.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La verge et la répréhension donnent la sagesse, mais le jeune garçon abandonné à lui-même fait honte à sa mère.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Quand les méchants se multiplient, la transgression se multiplie; mais les justes verront leur chute.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Corrige ton fils, et il te donnera du repos et procurera des délices à ton âme.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Quand il n’y a point de vision, le peuple est sans frein; mais bienheureux celui qui garde la loi!
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Un serviteur n’est pas corrigé par des paroles; car il comprend, mais il ne répond pas.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
As-tu vu un homme précipité dans ses paroles? Il y a plus d’espoir pour un sot que pour lui.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Celui qui gâte son serviteur dès sa jeunesse, le verra fils à la fin.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
L’homme colère excite les querelles, et l’homme qui se met en fureur abonde en transgressions.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
L’orgueil d’un homme l’abaisse, mais celui qui est humble d’esprit acquiert la gloire.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Qui partage avec un voleur hait son âme; il entend l’adjuration, et ne déclare pas [la chose].
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
La crainte des hommes tend un piège, mais qui se confie en l’Éternel est élevé dans une haute retraite.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Plusieurs cherchent la face du gouverneur, mais le juste jugement d’un homme vient de l’Éternel.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
L’homme inique est l’abomination des justes, et celui qui est droit dans sa voie, l’abomination du méchant.

< Mithali 29 >