< Mithali 29 >
1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
Celui qui est souvent réprimandé et qui raidit son cou sera détruit soudainement, sans aucun remède.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Quand les justes prospèrent, le peuple se réjouit; mais quand les méchants gouvernent, le peuple gémit.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
Celui qui aime la sagesse fait la joie de son père; mais un compagnon de prostituées dilapide sa richesse.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Le roi, par la justice, rend le pays stable, mais celui qui prend des pots-de-vin le démolit.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
Un homme qui flatte son prochain déploie un filet pour ses pieds.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
L'homme mauvais est pris au piège par son péché, mais les justes peuvent chanter et se réjouir.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Les justes se soucient de la justice pour les pauvres. Les méchants ne se soucient pas de la connaissance.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Les moqueurs agitent une ville, mais les hommes sages détournent la colère.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Si un homme sage va au tribunal avec un homme insensé, le fou se met en colère ou se moque, et il n'y a pas de paix.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Les sanguinaires détestent les hommes intègres; et ils recherchent la vie des honnêtes gens.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
L'imbécile évacue toute sa colère, mais un homme sage se maîtrise.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Si un dirigeant écoute les mensonges, tous ses fonctionnaires sont méchants.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Le pauvre et l'oppresseur ont ceci en commun: Yahvé donne la vue aux yeux des deux.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
Le roi qui juge équitablement les pauvres, son trône sera établi pour toujours.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
La verge de la correction donne la sagesse, mais un enfant laissé à lui-même fait honte à sa mère.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Quand les méchants augmentent, le péché augmente; mais les justes verront leur chute.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Corrige ton fils, et il te donnera la paix; oui, il apportera du plaisir à votre âme.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Là où il n'y a pas de révélation, le peuple se défait de toute contrainte; mais celui qui garde la loi est béni.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Un serviteur ne peut pas être corrigé par des mots. Bien qu'il comprenne, il ne répond pas.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Vois-tu un homme qui se hâte dans ses paroles? Il y a plus d'espoir pour un fou que pour lui.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Celui qui dorlote son serviteur dès sa jeunesse le fera devenir un fils à la fin.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
Un homme en colère suscite des querelles, et un homme courroucé abonde en péchés.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
L'orgueil d'un homme l'abaisse, mais celui qui a l'esprit humble gagne l'honneur.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Celui qui est complice d'un voleur est l'ennemi de sa propre âme. Il prête serment, mais n'ose pas témoigner.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
La crainte de l'homme s'avère être un piège, mais celui qui met sa confiance en Yahvé est en sécurité.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Beaucoup cherchent la faveur du chef, mais la justice d'un homme vient de Yahvé.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
L'homme malhonnête déteste les justes, et ceux qui sont droits dans leurs voies détestent les méchants.