< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
He that being often reproved stiffeneth his neck, suddenly shall be hurt, and there be no healing.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
When the righteous become great, the people rejoice, but, when a lawless man beareth rule, a people sigh.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
A man who loveth wisdom, gladdeneth his father, but, a companion of harlots, destroyeth wealth.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
A king, by justice, shall establish a land, —but, a man open to bribes, bringeth it to ruin.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
A man who flattereth his neighbour, spreadeth, a net, over his steps.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
In the transgression of a wicked man, is a snare, but, the righteous, doth shout in triumph and rejoice.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
The righteous doth acknowledge the plea of the poor, but, the lawless, regardeth not knowledge.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Men given to mockery, inflame a city, —but, wise men, turn away anger.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
A wise man pleading with a foolish man, whether he rage or laugh, there is no settlement.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Blood-thirsty men, hate the blameless man, and, as for the upright, they seek his life.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
All his anger, doth a dullard let go, but, a wise man, by keeping it back, stilleth it.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
When a ruler giveth heed to the word of falsehood, all his attendants, become lawless.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
The poor man and the man of usury, meet together, he that enlighteneth the eyes of them both, is Yahweh.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
When a king judgeth faithfully the poor, his throne, to futurity, shall be established.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
A rod with rebuke, giveth wisdom, but, a youth unrestrained, bringeth shame to his mother.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
When the lawless become great, transgression increaseth, but, the righteous, shall behold, their ruin.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Correct thy son, that he may give thee rest, that he may give delight to thy soul.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Where there is no vision, a people is let loose, but, he that keepeth instruction, how happy is he!
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
By words, a servant will not be corrected, though he perceiveth, yet is there no answer.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Thou hast seen a man hasty in his words, —there is, more hope of a dullard, than of him.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
He that dealeth tenderly with his servant from childhood, in his after life, shall have him for a son.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
A man given to anger, stirreth up strife, and, he that exceedeth in wrath, aboundeth in transgression.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
The loftiness of a man, layeth him low, —but, one of a lowly spirit, shall attain unto honour.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
He that shareth with a thief, hateth himself, an oath, he heareth, yet may not tell.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
The fear of man, setteth a snare, but, he that trusteth in Yahweh, shall be placed on high.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Many, seek the face of a ruler, but, from Yahweh, is the sentence of each one.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
An abomination to the righteous, is the man of perversity, and, an abomination to the lawless, is a man of straightforward way.

< Mithali 29 >