< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
A man that hardeneth his necke when he is rebuked, shall suddenly be destroyed and can not be cured.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
When the righteous are in authoritie, the people reioyce: but when the wicked beareth rule, the people sigh.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
A man that loueth wisdome, reioyceth his father: but he that feedeth harlots, wasteth his substance.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
A King by iudgement mainteineth ye countrey: but a man receiuing giftes, destroyeth it.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
A man that flattereth his neighbour, spreadeth a net for his steps.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
In the transgression of an euill man is his snare: but the righteous doeth sing and reioyce.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
The righteous knoweth the cause of the poore: but the wicked regardeth not knowledge.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Scornefull men bring a citie into a snare: but wise men turne away wrath.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
If a wise man contend with a foolish man, whether he be angry or laugh, there is no rest.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Bloodie men hate him that is vpright: but the iust haue care of his soule.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
A foole powreth out all his minde: but a wise man keepeth it in till afterward.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
Of a prince that hearkeneth to lyes, all his seruants are wicked.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
The poore and the vsurer meete together, and the Lord lighteneth both their eyes.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
A King that iudgeth the poore in trueth, his throne shalbe established for euer.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
The rodde and correction giue wisdome: but a childe set a libertie, maketh his mother ashamed.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
When the wicked are increased, transgression increaseth: but ye righteous shall see their fall.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Correct thy sonne and he will giue thee rest, and will giue pleasures to thy soule.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Where there is no vision, the people decay: but he that keepeth the Lawe, is blessed.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
A seruant will not be chastised with words: though he vnderstand, yet he will not answere.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Seest thou a man hastie in his matters? there is more hope of a foole, then of him.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
He that delicately bringeth vp his seruant from youth, at length he will be euen as his sone.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
An angrie man stirreth vp strife, and a furious man aboundeth in transgression.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
The pride of a man shall bring him lowe: but the humble in spirit shall enioy glory.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
He that is partner with a thiefe, hateth his owne soule: he heareth cursing, and declareth it not.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
The feare of man bringeth a snare: but he that trusteth in the Lord, shalbe exalted.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Many doe seeke the face of the ruler: but euery mans iudgement commeth from the Lord.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
A wicked man is abomination to the iust, and he that is vpright in his way, is abomination to the wicked.

< Mithali 29 >