< Mithali 29 >
1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
Anyone who goes on stubbornly rejecting many warnings will be suddenly destroyed, without hope of healing.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
When good people are in charge, everybody celebrates; but when the wicked rule, everybody groans.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
A man who loves wisdom makes his father happy, but one who visits prostitutes throws away his money.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
A king who rules justly makes the country secure, but one who asks for bribes will destroy it.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
Those who flatter their friends lay a net to trip them up.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
Evil people are trapped by their own sins, but those who do right sing and celebrate.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Good people care about treating the poor fairly, but the wicked don't think about it at all.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Cynical people can inflame a whole city, but the wise calm angry people down.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
When a wise man takes a stupid man to court, there's raging and ridicule, but nothing is settled.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
Murderers hate people of integrity, but those who live right try to help them.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
Stupid people let all their anger out, while wise people quietly hold it in.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
A ruler who listens to lies will have nothing but wicked officials.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Poor people and their oppressors have this in common: the Lord gives life to all of them.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
If a king judges the poor fairly, he will have a long rule.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
Discipline and correction provide wisdom, but a son left undisciplined is an embarrassment to his mother.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
When the wicked are in power, sin increases; but the good will see their downfall.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Discipline your children and they won't give you any worries; they will make you very happy.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Without a revelation from God, the people go out of control, but those who keep the law are happy.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
A servant can't be disciplined by words alone; though they understand, they don't follow what they're told.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Have you seen a man who speaks without thinking? There's more hope for stupid people than for him!
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
A servant indulged from childhood will in the end become unmanageable.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
Angry people stir up trouble, those with short tempers commit many sins.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
If you're proud, you'll be humiliated; but if you're humble, you'll be honored.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
A thief's partner hates his life; even under the threat of being cursed he can't tell the truth.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
Being afraid of people traps you, but if you trust in the Lord you're safe.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Many people look for favors from a ruler, but justice comes from the Lord.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Good people hate those who are unjust; the wicked hate those who do what's right.