< Mithali 29 >

1 Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
Hvo Nakken gør stiv, skønt revset tit, han knuses brat uden Lægedom.
2 Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
Er der mange retfærdige, glædes Folket, men råder de gudløse, sukker Folket.
3 Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
Hvo Visdom elsker, glæder sin Fader, hvo Skøger omgås, bortødsler Gods.
4 Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
Kongen grundfæster Landet med Ret, en Udsuger lægger det øde.
5 Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
Mand, der smigrer sin Næste, breder et Net for hans Fod.
6 Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
I sin Brøde hildes den onde, den retfærdige jubler af Glæde.
7 Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
Den retfærdige kender de ringes Retssag; den gudløse skønner intet.
8 Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
Spottere ophidser Byen, men Vismænd, de stiller Vrede.
9 Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
Går Vismand i Rette med Dåre, vredes og ler han, alt preller af.
10 Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
De blodtørstige hader lydefri Mand, de retsindige tager sig af ham.
11 Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
En Tåbe slipper al sin Voldsomhed løs, Vismand stiller den omsider.
12 Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
En Fyrste, som lytter til Løgnetale, får lufter gudløse Tjenere.
13 Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
Fattigmand og Blodsuger mødes, HERREN giver begges Øjne Glans.
14 Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
En Konge, der dømmer de ringe med Ret, hans Trone står fast evindelig.
15 Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
Ris og Revselse, det giver Visdom, uvorn Dreng gør sin Moder Skam.
16 Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
Bliver mange gudløse tiltager Synd; retfærdige ser med Fryd deres Fald.
17 Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
Tugt din Søn, så kvæger han dig og bringer din Sjæl, hvad der smager.
18 Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
Uden Syner forvildes et Folk; salig den, der vogter på Loven.
19 Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
Med Ord lader Træl sig ikke tugte, han fatter dem vel, men adlyder ikke.
20 Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
Ser du en Mand, der er hastig til Tale, for en Tåbe er der snarere Håb end for ham.
21 Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
Forvænner man sin Træl fra ung, vil han til sidst være Herre.
22 Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
Hidsig Mand vækker Strid, vredladen Mand gør megen Synd.
23 Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
Et Menneskes Hovmod ydmyger ham, den ydmyge opnår Ære.
24 Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
Hæleren hader sit Liv, han hører Forbandelsen, men melder intet.
25 Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
Frygt for Mennesker leder i Snare, men den, der stoler på HERREN, er bjærget.
26 Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
Mange søger en Fyrstes Gunst; Mands Ret er dog fra HERREN.
27 Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.
Urettens Mand er retfærdiges Gru, hvo redeligt vandrer, gudløses Gru.

< Mithali 29 >