< Mithali 28 >

1 Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
HUYE el impío sin que nadie lo persiga: mas el justo está confiado como un leoncillo.
2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
Por la rebelión de la tierra sus príncipes son muchos: mas por el hombre entendido y sabio permanecerá sin mutación.
3 Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
El hombre pobre y robador de los pobres, es lluvia de avenida y sin pan.
4 Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
Los que dejan la ley, alaban á los impíos: mas los que la guardan, contenderán con ellos.
5 Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
Los hombres malos no entienden el juicio: mas los que buscan á Jehová, entienden todas las cosas.
6 Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
Mejor es el pobre que camina en su integridad, que el de perversos caminos, y rico.
7 Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
El que guarda la ley es hijo prudente: mas el que es compañero de glotones, avergüenza á su padre.
8 Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
El que aumenta sus riquezas con usura y crecido interés, para que se dé á los pobres lo allega.
9 Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
El que aparta su oído para no oir la ley, su oración también es abominable.
10 Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
El que hace errar á los rectos por el mal camino, él caerá en su misma sima: mas los perfectos heredarán el bien.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
El hombre rico es sabio en su opinión: mas el pobre entendido lo examinará.
12 Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
Cuando los justos se alegran, grande es la gloria; mas cuando los impíos son levantados, es buscado el hombre.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
El que encubre sus pecados, no prosperará: mas el que los confiesa y se aparta, alcanzará misericordia.
14 Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
Bienaventurado el hombre que siempre está temeroso: mas el que endurece su corazón, caerá en mal.
15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
León rugiente y oso hambriento, [es] el príncipe impío sobre el pueblo pobre.
16 Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
El príncipe falto de entendimiento multiplicará los agravios: [mas] el que aborrece la avaricia, prolongará sus días.
17 Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
El hombre que hace violencia con sangre de persona, huirá hasta el sepulcro, y nadie le detendrá.
18 Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
El que en integridad camina, será salvo; mas el de perversos caminos caerá en alguno.
19 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
El que labra su tierra, se hartará de pan: mas el que sigue los ociosos, se hartará de pobreza.
20 Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
El hombre de verdad tendrá muchas bendiciones: mas el que se apresura á enriquecer, no será sin culpa.
21 Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
Tener acepción de personas, no es bueno: hasta por un bocado de pan prevaricará el hombre.
22 Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
Apresúrase á ser rico el hombre de mal ojo; y no conoce que le ha de venir pobreza.
23 Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
El que reprende al hombre, hallará después mayor gracia que el que lisonjea con la lengua.
24 Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
El que roba á su padre ó á su madre, y dice que no es maldad, compañero es del hombre destruidor.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
El altivo de ánimo suscita contiendas: mas el que en Jehová confía, medrará.
26 Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
El que confía en su corazón es necio; mas el que camina en sabiduría, será salvo.
27 Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
El que da al pobre, no tendrá pobreza: mas el que aparta sus ojos, tendrá muchas maldiciones.
28 Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.
Cuando los impíos son levantados, esconderáse el hombre: mas cuando perecen, los justos se multiplican.

< Mithali 28 >