< Mithali 28 >

1 Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
Huye el impío sin que nadie lo persiga, Pero como león está confiado el justo.
2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
Por la rebelión de la tierra sus jefes son muchos, Pero por el hombre entendido y sabio permanece estable.
3 Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
El hombre pobre que explota a los indigentes Es como lluvia torrencial que no deja pan.
4 Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
Los que abandonan la Ley alaban al impío. Los que la guardan contienden con ellos.
5 Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
Los perversos no entienden la justicia, Pero el que busca a Yavé lo entiende todo.
6 Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
Mejor es el pobre que anda en su integridad, Que rico de caminos torcidos.
7 Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
El que observa la Ley es hijo inteligente, El que se reúne con glotones avergüenza a su padre.
8 Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
El que aumenta su fortuna con interés y usura Acumula para el que se compadece de los pobres.
9 Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Al que aparta su oído para no oír la Ley, Aun su oración es una repugnancia.
10 Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
El que extravía al recto por el mal camino Caerá en su propia fosa, Pero los íntegros heredarán el bien.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
El hombre rico es sabio en su propia opinión, Pero el entendido pobre lo escudriña.
12 Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
Cuando triunfa el justo hay gran esplendor, Cuando se yerguen los impíos, los hombres se esconden.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
El que encubre sus pecados no prosperará, Pero el que los confiesa y se aparta alcanzará misericordia.
14 Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
¡Inmensamente feliz es el hombre que teme siempre! Pero el que endurece su corazón caerá en la desgracia.
15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
León rugiente y oso hambriento, Es el gobernante impío sobre un pueblo pobre.
16 Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
El gobernante falto de entendimiento aumenta la extorsión, Pero el que aborrece la avaricia alargará sus días.
17 Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
El hombre culpable de homicidio hacia la fosa huye. ¡Nadie lo detenga!
18 Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
El que anda en integridad será librado, Pero el que oscila entre dos caminos caerá de repente.
19 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
El que labra su tierra se saciará de pan, Pero el que persigue vanidades se hartará de pobreza.
20 Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
El hombre leal tendrá muchas bendiciones, Pero el que se apresura a enriquecerse no quedará impune.
21 Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
Hacer acepción de personas no es bueno, Pero, ¡hasta por un bocado de pan puede transgredir un hombre!
22 Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
El hombre de mirada desleal se afana por enriquecer, Y no sabe que lo alcanzará la miseria.
23 Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
El que reprende al hombre hallará mayor gracia Que el de boca lisonjera.
24 Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
El que roba a padre o madre y dice que no es pecado, Es compañero del destructor.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
El arrogante suscita contiendas, Pero el que confía en Yavé prosperará.
26 Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
El que confía en su propio corazón es un necio, Pero el que anda en sabiduría será librado.
27 Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
El que da al pobre no tendrá necesidad, Pero el que aparta de él sus ojos tendrá muchas maldiciones.
28 Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.
Cuando se levantan los perversos, los hombres se esconden, Pero cuando perecen, aumentan los justos.

< Mithali 28 >