< Mithali 28 >
1 Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
Les méchants fuient quand personne ne les poursuit; mais les justes sont aussi audacieux qu'un lion.
2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
Dans la rébellion, un pays a plusieurs chefs, mais l'ordre est maintenu par un homme de compréhension et de connaissance.
3 Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
Un homme dans le besoin qui opprime les pauvres est comme une pluie battante qui ne laisse aucune récolte.
4 Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
Ceux qui abandonnent la loi louent les méchants; mais ceux qui gardent la loi les combattent.
5 Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
Les hommes mauvais ne comprennent pas la justice; mais ceux qui cherchent Yahvé le comprennent parfaitement.
6 Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
Meilleur est le pauvre qui marche dans son intégrité que celui qui est pervers dans ses voies, et il est riche.
7 Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
Celui qui observe la loi est un fils sage; mais celui qui est le compagnon des gloutons fait honte à son père.
8 Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
Celui qui augmente sa richesse par des intérêts excessifs le recueille pour celui qui a pitié des pauvres.
9 Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Celui qui détourne son oreille pour ne pas entendre la loi, même sa prière est une abomination.
10 Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
Celui qui fait égarer les justes dans une voie mauvaise, il tombera dans son propre piège; mais les irréprochables hériteront du bien.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
Le riche est sage à ses propres yeux; mais le pauvre qui a de l'intelligence voit à travers lui.
12 Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
Quand les justes triomphent, il y a une grande gloire; mais quand les méchants se lèvent, les hommes se cachent.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
Celui qui cache ses péchés ne prospère pas, mais celui qui les confesse et y renonce trouve la miséricorde.
14 Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
Heureux l'homme qui craint toujours; mais celui qui endurcit son cœur tombe dans le malheur.
15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
Comme un lion qui rugit ou un ours qui charge, ainsi qu'un souverain méchant sur des gens sans défense.
16 Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
Un dirigeant tyrannique manque de jugement. Celui qui déteste le gain mal acquis aura de longs jours.
17 Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
L'homme qui est tourmenté par la culpabilité du sang sera un fugitif jusqu'à la mort. Personne ne le soutiendra.
18 Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
Celui qui marche sans reproche est en sécurité; mais celui qui a des manières perverses tombera soudainement.
19 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
Celui qui travaille sa terre aura de la nourriture en abondance; mais celui qui poursuit des fantasmes aura son lot de pauvreté.
20 Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
Un homme fidèle est riche en bénédictions; mais celui qui est désireux de s'enrichir ne restera pas impuni.
21 Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
Faire preuve de partialité n'est pas bon, mais un homme fera le mal pour un morceau de pain.
22 Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
Un homme avare se précipite après les richesses, et ne sait pas que la pauvreté l'attend.
23 Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
Celui qui réprimande un homme trouvera plus de faveur par la suite. que celui qui flatte avec la langue.
24 Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
Celui qui vole son père ou sa mère et dit: « Ce n'est pas mal ». est un partenaire avec un destructeur.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
Celui qui est avide suscite des querelles; mais celui qui se confie en Yahvé prospérera.
26 Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
Celui qui se confie en lui-même est un insensé; mais celui qui marche dans la sagesse est en sécurité.
27 Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
Celui qui donne aux pauvres ne manque de rien; mais celui qui ferme les yeux aura de nombreuses malédictions.
28 Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.
Quand les méchants se lèvent, les hommes se cachent; mais quand ils périssent, les justes prospèrent.