< Mithali 28 >
1 Mtu mwovu hukimbia ingawa hakuna yeyote anayemfukuza, bali wenye haki ni wajasiri kama simba.
The impious flees, though no one pursues. But the just, like a confident lion, shall be without dread.
2 Wakati nchi inapokuwa na uasi, inakuwa na viongozi wengi, bali mwenye ufahamu na maarifa hudumisha utaratibu.
Because of the sins of the land, it has many princes. And because of the wisdom of a man, and the knowledge of those things that are said, the life of the leader shall be prolonged.
3 Mtu maskini amwoneaye yeye aliye maskini zaidi ni kama mvua ya dhoruba isiyosaza mazao.
A poor man slandering the poor is like a violent rainstorm in advance of a famine.
4 Wale waiachao sheria huwasifu waovu, bali wale waishikao sheria huwapinga.
Those who abandon the law praise the impious. Those who guard it are inflamed against him.
5 Watu wabaya hawaelewi haki, bali wale wamtafutao Bwana wanaielewa kikamilifu.
Evil men do not intend judgment. But those who inquire after the Lord turn their souls toward all things.
6 Afadhali maskini ambaye mwenendo wake hauna lawama kuliko tajiri ambaye njia zake ni potovu.
Better is the pauper walking in his simplicity, than the rich walking in ways of depravity.
7 Yeye ashikaye sheria ni mwana mwenye ufahamu, bali rafiki wa walafi humwaibisha baba yake.
Whoever keeps the law is a wise son. But whoever feeds gluttons brings shame to his father.
8 Yeye aongezaye utajiri wake kwa riba kubwa mno hukusanya kwa ajili ya mwingine, ambaye atawahurumia maskini.
Whoever piles up riches by usury and profit gathers them for him who will give freely to the poor.
9 Kama mtu yeyote akikataa kusikia sheria, hata maombi yake ni chukizo.
Whoever turns away his ears from listening to the law: his prayer will be detestable.
10 Yeye ambaye humwongoza mwenye haki kwenye mapito mabaya, ataanguka kwenye mtego wake mwenyewe, bali wasio na lawama watapokea urithi mwema.
Whoever deceives the just in a malicious way will fall into his own perdition. And the simple shall possess his goods.
11 Mtu tajiri anaweza kuwa na hekima machoni pake mwenyewe, bali mtu maskini mwenye ufahamu atamfichua.
The rich one seems wise to himself. But the poor one, being prudent, shall evaluate him.
12 Mwenye haki ashindapo, kuna furaha kubwa, bali waovu watawalapo, watu hujificha.
In the exultation of the just, there is great glory. When the impious reign, men are brought to ruin.
13 Yeye afichaye dhambi zake hatafanikiwa, bali yeyote aziungamaye na kuziacha hupata rehema.
Whoever hides his crimes will not be guided. But whoever will have confessed and abandoned them shall overtake mercy.
14 Amebarikiwa mtu ambaye siku zote humcha Bwana, bali yeye afanyaye moyo wake kuwa mgumu huangukia kwenye taabu.
Blessed is the man who is ever fearful. Yet truly, whoever is hardened in mind will fall into evil.
15 Kama simba angurumaye au dubu ashambuliaye, ndivyo alivyo mtu mwovu atawalaye wanyonge.
An impious leader over a poor people is like a roaring lion and a hungry bear.
16 Mtawala dhalimu hana akili, bali yeye achukiaye mapato ya udhalimu atafurahia maisha marefu.
A leader destitute of prudence will oppress many through false accusations. But whoever hates avarice shall prolong his days.
17 Mtu mwenye kusumbuliwa na hatia ya kuua atakuwa mtoro mpaka kufa; mtu yeyote na asimsaidie.
A man who slanders the blood of a life, even if he flees to the pit, no one will tolerate him.
18 Yeye ambaye mwenendo wake hauna lawama hulindwa salama, bali yeye ambaye njia zake ni potovu ataanguka ghafula.
Whoever walks simply shall be saved. Whoever is perverse in his steps will fall all at once.
19 Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yule afuataye mambo ya upuzi atakuwa na umaskini wa kumtosha.
Whoever works his land shall be satisfied with bread. But whoever pursues leisure will be filled with need.
20 Mtu mwaminifu atabarikiwa sana, bali yeye atamaniye kupata utajiri kwa haraka hataacha kuadhibiwa.
A faithful man shall be greatly praised. But whoever rushes to become rich will not be innocent.
21 Kuonyesha upendeleo si vizuri, hata hivyo mtu atafanya kosa kwa kipande cha mkate.
Whoever shows favoritism in judgment does not do well; even if it is for a morsel of bread, he forsakes the truth.
22 Mtu mchoyo ana tamaa ya kupata utajiri, naye hana habari kuwa umaskini unamngojea.
A man who hurries to become rich, and who envies others, does not know that destitution will overwhelm him.
23 Yeye amkemeaye mtu mwishoni hupata kibali zaidi, kuliko mwenye maneno ya kusifu isivyostahili.
Whoever corrects a man, afterward he shall find favor with him, more so than he who deceives him with a flattering tongue.
24 Yeye amwibiaye babaye au mamaye na kusema, “Si kosa,” yeye ni mwenzi wa yule aharibuye.
Whoever takes away anything from his father or mother, and who says, “This is not a sin,” is the associate of a murderer.
25 Mtu mwenye tamaa huchochea fitina, bali yule amtegemeaye Bwana atafanikiwa.
Whoever boasts and enlarges himself stirs up conflicts. Yet truly, whoever trusts in the Lord will be healed.
26 Yeye ajitumainiaye mwenyewe ni mpumbavu, bali yeye atembeaye katika hekima hulindwa salama.
Whoever trusts in his own heart is a fool. But whoever treads wisely, the same shall be saved.
27 Yeye ampaye maskini hatapungukiwa na kitu chochote, bali yeye awafumbiaye maskini macho hupata laana nyingi.
Whoever gives to the poor shall not be in need. Whoever despises his petition will suffer scarcity.
28 Wakati waovu watawalapo, watu huenda mafichoni, bali waovu wanapoangamia, wenye haki hufanikiwa.
When the impious rise up, men will hide themselves. When they perish, the just shall be multiplied.