< Mithali 27 >

1 Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
NO te jactes del día de mañana; porque no sabes qué dará de sí el día.
2 Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
Alábete el extraño, y no tu boca; el ajeno, y no tus labios.
3 Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
Pesada es la piedra, y la arena pesa; mas la ira del necio es más pesada que ambas cosas.
4 Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
Cruel es la ira, é impetuoso el furor; mas ¿quién parará delante de la envidia?
5 Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
Mejor es reprensión manifiesta que amor oculto.
6 Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
Fieles son las heridas del que ama; pero importunos los besos del que aborrece.
7 Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
El alma harta huella el panal de miel; mas al alma hambrienta todo lo amargo es dulce.
8 Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
Cual ave que se va de su nido, tal es el hombre que se va de su lugar.
9 Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
El ungüento y el perfume alegran el corazón: y el amigo al hombre con el cordial consejo.
10 Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
No dejes á tu amigo, ni al amigo de tu padre; ni entres en casa de tu hermano el día de tu aflicción: mejor es el vecino cerca que el hermano lejano.
11 Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
Sé sabio, hijo mío, y alegra mi corazón, y tendré qué responder al que me deshonrare.
12 Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
El avisado ve el mal, [y] escóndese; [mas] los simples pasan, [y] llevan el daño.
13 Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
Quítale su ropa al que fió al extraño; y [al que fió] á la extraña, tómale prenda.
14 Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
El que bendice á su amigo en alta voz, madrugando de mañana, por maldición se le contará.
15 Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
Gotera continua en tiempo de lluvia, y la mujer rencillosa, son semejantes:
16 Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
El que pretende contenerla, arresta el viento: ó el aceite en su mano derecha.
17 Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
Hierro con hierro se aguza; y el hombre aguza el rostro de su amigo.
18 Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
El que guarda la higuera, comerá su fruto; y el que guarda á su señor, será honrado.
19 Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
Como un agua se parece á otra, así el corazón del hombre al otro.
20 Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
El sepulcro y la perdición nunca se hartan: así los ojos del hombre nunca están satisfechos. (Sheol h7585)
21 Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
El crisol [prueba] la plata, y la hornaza el oro: y al hombre la boca del que lo alaba.
22 Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
Aunque majes al necio en un mortero entre granos de trigo á pisón majados, no se quitará de él su necedad.
23 Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
Considera atentamente el aspecto de tus ovejas; pon tu corazón á tus rebaños:
24 Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
Porque las riquezas no son para siempre; ¿y [será] la corona para perpetuas generaciones?
25 Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
Saldrá la grama, aparecerá la hierba, y segaránse las hierbas de los montes.
26 wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
Los corderos para tus vestidos, y los cabritos para el precio del campo:
27 Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.
Y abundancia de leche de las cabras para tu mantenimiento, y para mantenimiento de tu casa, y para sustento de tus criadas.

< Mithali 27 >